• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

ZIARA YA WAZIRI WA NCHI OFISI YA MAKAMU WA RAIS MUUNGANO NA MAZINMGIRA , 23/1/2022

Posted on: February 6th, 2022

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamo wa Rais, Muungano na Mazingira, Mhe. Suleiman Jafo, ameiagiza Kampuni ya Mgodi, Katavi (Katavi Mining CO. Ltd ) kushughulikia kwa haraka upatikanaji wa Cheti cha Mazingira na Uwepo wa Mfumo wa Majitaka (TSF) ndani ya mwaka 1 kuanzia Januari 2022.

Mhe. Jafo ametoa agizo hilo jana baada ya kufanya ukaguzi katika Kampuni ya Mgodi Katavi, na kugundua kuwa mgodi huo unaendesha shughuli zake bila cheti cha mazingira ambacho walipaswa kuwa nacho kabla ya kuweka miundombinu mbali mbali katika eneo la mgodi.

“Hapa kuna changamoto ya kimazingira kwa sababu mgodi hauna cheti cha mazingira wala mfumo wa majitaka(TSF),  hivyo kutokuwepo kwa vigezo hivyo 2 vya usafi na utunzaji wa mazingira katika eneo la mgodi, ni kosa na uchafuzi wa mazingira, Mgodi unapaswa kutozwa faini kubwa.” Mhe. Jafo amesema.

Kufuatia mapungufu hayo, kiongozi huyo ameuagiza uongozi wa Mgodi kufanya marekebisho ya dosari hizo na kukamiisha ndani ya mwaka 1 kuanzia Januari 2022 hadi Januari 2023.

Mhe. Jafo ameonya kuwa kutokuzingatiwa kwa vigezo hivyo, kuna athari za uchafuzi wa mazingira ikiwemo kuchafua vyanzo vya maji na taka sumu kwenda kwenye ardhi jambo ambalo ni hatari kwa maisha ya binadamu na viumbe wengine.

Kaimu Mtendaji wa Kampuni ya Mgodi, Katavi Mining CO. Ltd Bw. Twalib Mohamed amesema yeye pamoja na uongozi wa Mgodi, watatekeleza kwa haraka sana maagizo yote yaliyotolewa na waziri mwenye dhamana ya Mazingira nchini Tanzania ili kuendana na matakwa ya sheria ya mazingira.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe. Mwanamvua Mrindoko amemhakikishia, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamo wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe. S. Jafo, kuwa yeye na viongozi wenzake wataendelea kuwasimamia na kuwahimiza wawekezaji wote katika mkoa wake kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu zinazosimamia mazingira.

Mhe. Jafo amewapongeza wawekezaji wa Kampuni ya Mgodi, Katavi kwa uwekezaji mkubwa katika nchi ya Tanzania, kwa kutengeneza ajira kwa watanzania,kuipatia serikali ya Tanzania mapato yake na kutoa michango mbali mbali kwa jamii.    

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • RATIBA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI - MWAKA 2025 April 28, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA SEKTA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI MKOA WA KATAVI August 27, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA SEKTA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI MKOA WA KATAVI August 27, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AHIMIZA AMANI NA USHIRIKIANO KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025.

    September 01, 2025
  • MFUMO WA E - MABORESHO KUIMARISHA UTENDAJI KWA WATUMISHI WA UMMA.

    August 26, 2025
  • MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA YAFIKIA TAMATI, DC BUSWELU AWASISITIZA UZALENDO

    August 26, 2025
  • VIJANA WA HALMASHAURI YA TANGANYIKA WAJITOKEZA KWA WINGI KATIKA KONGAMANO LA ELIMU NA MAPOKEO YA MWENGE WA UHURU.

    August 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved