• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

RAS MSOVELA AWATAKA WATUMISHI WA UMMA WILAYA YA TANGANYIKA KUWA MFANO WA KUIGWA, KUJENGA HUDUMA BORA, UWAZI NA UWAJIBIKAJI.

Posted on: December 3rd, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Bw. Albert Msovela, ametoa maelekezo makali kwa watumishi wa umma wa Wilaya ya Tanganyika, akisisitiza umuhimu wa uwajibikaji, uadilifu, mshikamano na utoaji huduma bora kwa wananchi.


Akiweka mkazo kwenye utawala bora, RAS Msovela amewaagiza Watendaji wa Kata na Vijiji kuhakikisha vikao vya kisheria vinafanyika kila wiki na taarifa za utekelezaji zinawasilishwa kwa Mkurugenzi kwa mujibu wa taratibu. Amesema malalamiko mengi kutoka kwa wananchi yanafaa kutatuliwa katika ngazi hizo za chini ili kupunguza mzigo katika mamlaka za juu.


Amesisitiza pia kuimarishwa kwa ukusanyaji wa mapato ya ndani, akizitaka halmashauri kuongeza kasi ya usimamizi wa vyanzo vya mapato ili kufikia malengo ya mwaka wa fedha na kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


Akizungumzia mwongozo wa Serikali kuhusu utoaji huduma kwa wananchi, Bw. Msovela amewakumbusha watumishi kuimarisha mahusiano chanya na wananchi kwa kutumia weledi, uwazi na kujenga mtiririko mzuri wa huduma kwa kila ngazi.


"Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameagiza turejeshe tabasamu kwa wananchi, hivyo ni wajibu wetu kujenga mfumo unaorahisisha kuwafikia wananchi katika maeneo yote," amesema RAS Msovela.


Aidha, RAS Msovela amewataka watumishi kutumia kwa umakini makundi ya mawasiliano ya kikazi na kuzingatia uadilifu katika maamuzi na vitendo vyao vya kila siku, akibainisha kuwa umoja na kuepuka majungu ni msingi wa ufanisi katika utumishi wa umma.


Katika hitimisho la maelekezo yake, amezitaka idara za kilimo kuimarisha huduma kwa wakulima kupitia uwepo wa karibu wa Maafisa Ugani mashambani, akibainisha kuwa mashamba ndiyo eneo la msingi la utoaji huduma za kitaalam.


Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi – Sehemu ya Utawala na Rasilimali Watu, Bi. Cresensia Joseph, amewataka watumishi kuwa mfano wa kuigwa katika utendaji wao wa kila siku, akisisitiza nidhamu, uwajibikaji, uaminifu na utekelezaji wa maelekezo ya Serikali. Amesema uadilifu na weledi wa watumishi unajenga taswira chanya ya utumishi wa umma na kuongeza imani ya wananchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • RATIBA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI - MWAKA 2025 April 28, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA SEKTA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI MKOA WA KATAVI August 27, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA SEKTA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI MKOA WA KATAVI August 27, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RAS MSOVELA AWATAKA WATUMISHI WA UMMA WILAYA YA TANGANYIKA KUWA MFANO WA KUIGWA, KUJENGA HUDUMA BORA, UWAZI NA UWAJIBIKAJI.

    December 03, 2025
  • RAS MSOVELA AONGOZA BARAZA LA KWANZA LA MADIWANI MLELE, ASISITIZA UWAZIBIKAJI NA UAMINIFU KATIKA UTENDAJI.

    December 02, 2025
  • BARAZA LAMPITISHA MHE. ATHUMANI FIMBO KUWA MWENYEKITI H/W NSIMBO, RAS MSOVELA AWATAKA MADIWANI KUZINGATIA KANUNI NA TARATIBU.

    December 02, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII KATAVI WAPEWA NGUVU MPYA KUFUNGUA FURSA ZA ZABUNI KWA MAKUNDI MAALUM.

    November 27, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved