• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

RAS MSOVELA AONGOZA BARAZA LA KWANZA LA MADIWANI MLELE, ASISITIZA UWAZIBIKAJI NA UAMINIFU KATIKA UTENDAJI.

Posted on: December 2nd, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Bw. Albert Msovela, jana desemba 02, 2025 alifungua rasmi Baraza la Kwanza la Madiwani Wilaya ya Mlele na kusisitiza kwa kina umuhimu wa kufanya kazi kwa misingi ya uwajibikaji katika kila ngazi ya utumishi. Amesema kuwa serikali inahitaji watendaji wanaotenda kazi kwa uaminifu, kasi, na matokeo yanayoweza kupimika.


Akizungumza mbele ya madiwani na wataalamu wa halmashauri, Bw. Msovela amesema miradi mingi ya kimkakati inatekelezwa wilayani Mlele, hivyo kunahitajika ufuatiliaji makini na usimamizi wenye weledi ili kuhakikisha thamani ya fedha inaonekana na wananchi wanapata huduma stahiki kwa wakati.

Ameeleza kuwa nidhamu ya kazi, uwazi na kuzingatia sheria, kanuni na taratibu ni misingi isiyopaswa kupuuzwa, kwani ndiyo inayoimarisha taswira ya serikali na kuongeza imani ya wananchi kwa viongozi wao. Msovela amewataka madiwani kuwa mstari wa mbele katika kusimamia maamuzi ya baraza kwa masilahi ya wananchi, badala ya kutanguliza masuala ya kibinafsi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Mlele, Mhe. Majid Mwanga, amesisitiza umuhimu wa kudumisha uhusiano mzuri kati ya watumishi wa halmashauri na waheshimiwa madiwani. Amesema kuwa mara nyingi ucheleweshaji wa maendeleo hutokana na ukosefu wa maelewano, jambo ambalo linaepukika endapo pande zote zitajenga mawasiliano mazuri.

Mhe. Mwanga amesisitiza kuwa madiwani na watumishi wanapaswa kufanya kazi kama timu moja, wakiheshimiana na kushirikiana katika kupanga, kutekeleza na kufuatilia miradi ya maendeleo. Amesema kuwa ushirikiano ndio msingi wa kuimarisha utoaji wa huduma, kuongeza ufanisi wa miradi na kuleta matokeo chanya kwa wananchi.

Amehitimisha kwa kutoa wito wa kuondoa tofauti ndogo ndogo za kiutendaji na kuwekeza kwenye majadiliano yenye kujenga, ili wilaya iendelee kupiga hatua na kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • RATIBA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI - MWAKA 2025 April 28, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA SEKTA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI MKOA WA KATAVI August 27, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA SEKTA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI MKOA WA KATAVI August 27, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RAS MSOVELA AWATAKA WATUMISHI WA UMMA WILAYA YA TANGANYIKA KUWA MFANO WA KUIGWA, KUJENGA HUDUMA BORA, UWAZI NA UWAJIBIKAJI.

    December 03, 2025
  • RAS MSOVELA AONGOZA BARAZA LA KWANZA LA MADIWANI MLELE, ASISITIZA UWAZIBIKAJI NA UAMINIFU KATIKA UTENDAJI.

    December 02, 2025
  • BARAZA LAMPITISHA MHE. ATHUMANI FIMBO KUWA MWENYEKITI H/W NSIMBO, RAS MSOVELA AWATAKA MADIWANI KUZINGATIA KANUNI NA TARATIBU.

    December 02, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII KATAVI WAPEWA NGUVU MPYA KUFUNGUA FURSA ZA ZABUNI KWA MAKUNDI MAALUM.

    November 27, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved