• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

BARAZA LAMPITISHA MHE. ATHUMANI FIMBO KUWA MWENYEKITI H/W NSIMBO, RAS MSOVELA AWATAKA MADIWANI KUZINGATIA KANUNI NA TARATIBU.

Posted on: December 2nd, 2025

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, mkoani Katavi, limempitisha Diwani wa Kata ya Sitalike, Mhe. Athumani Juma Fimbo, kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo baada ya kupata kura 13 kati ya kura zote 13 katika uchaguzi uliofanyika leo.

Akizungumza katika kikao hicho, Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Bw. Albert Msovela, ambaye alikuwa mgeni rasmi, amewapongeza madiwani kwa umoja waliouonyesha katika kuchagua uongozi mpya. Aidha, amewahimiza kuhakikisha kuwa katika kutekeleza majukumu yao, wanazingatia kanuni, taratibu na sheria ili kuongeza ufanisi na kuimarisha utawala bora ndani ya Halmashauri.

“Niwaombe madiwani mhakikishe mnazingatia kanuni, taratibu na sheria katika kila hatua ya utendaji wenu. Ushirikiano kati yenu na watumishi wa Halmashauri ni msingi muhimu wa kuleta maendeleo kwa wananchi.” Amesema Bw. Msovela.


Aidha, Bw. Msovela amewataka waheshimiwa madiwani kuhakikisha wanasimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi ya maendeleo ndani ya Halmashauri, akisisitiza kuwa miradi hiyo ndiyo kielelezo cha ufanisi wa Serikali katika ngazi za chini. Amesema usimamizi makini, ufuatiliaji wa mara kwa mara na uwajibikaji ndiyo nguzo zitakazohakikisha wananchi wanapata matokeo halisi ya uwekezaji unaofanywa na Serikali.

Bw. Msovela pia ameipongeza Menejimenti ya Halmashauri inayoongozwa na Mkurugenzi Bi. Christina Bunini pamoja na Kamati ya CMT kwa hatua kubwa zilizopigwa katika kusimamia na kutekeleza miradi ya maendeleo tangu kuvunjwa kwa Baraza lililopita.


Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Mhe. Jamila Yusuph, amewataka waheshimiwa madiwani kusimamia kikamilifu mikopo ya asilimia 10, kuhamasisha suala la kilimo, na kuhakikisha ukusanyaji wa mapato unafanyika kwa ufanisi ili kuongeza mapato ya ndani ya Halmashauri.


Akizungumza mara baada ya kuthibitishwa, Mhe.Fimbo ameahidi kufanya kazi kwa karibu na madiwani wenzake ili kuleta maendeleo kupitia utekelezaji wa sera walizoahidi wakati wa kampeni za uchaguzi wa Oktoba mwaka huu.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • RATIBA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI - MWAKA 2025 April 28, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA SEKTA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI MKOA WA KATAVI August 27, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA SEKTA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI MKOA WA KATAVI August 27, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RAS MSOVELA AWATAKA WATUMISHI WA UMMA WILAYA YA TANGANYIKA KUWA MFANO WA KUIGWA, KUJENGA HUDUMA BORA, UWAZI NA UWAJIBIKAJI.

    December 03, 2025
  • RAS MSOVELA AONGOZA BARAZA LA KWANZA LA MADIWANI MLELE, ASISITIZA UWAZIBIKAJI NA UAMINIFU KATIKA UTENDAJI.

    December 02, 2025
  • BARAZA LAMPITISHA MHE. ATHUMANI FIMBO KUWA MWENYEKITI H/W NSIMBO, RAS MSOVELA AWATAKA MADIWANI KUZINGATIA KANUNI NA TARATIBU.

    December 02, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII KATAVI WAPEWA NGUVU MPYA KUFUNGUA FURSA ZA ZABUNI KWA MAKUNDI MAALUM.

    November 27, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved