• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

Hotuba

MSIMAMO WA SERIKALI KUHUSU WATANZANIA WAPYA WALIOPEWA URAIA KATIKA MAKAZI YA KATUMBA, MISHAMO NA ULYANKULU.

 

Serikali imeweka wazi msimamo wake kuwa inaweza kuwafutia uraia watanzania wapya waliopewa uraia wale ambao walikuwa wakimbizi wanaoishi makazi ya katumba Mishamo na Ulyankulu iwapo wataonekana kushindwa kufuata sheria za nchi na kujihusisha na vitendo vya uharifu na uvunjifu wa sheria za nchi na kusisitiza vitendo vya ubaguzi wenyewe kwa wenyewe ubaguzi wa kitabaka kubaguana kisiasa,kidini na kwa namna yeyote hawawezi kuvumiliwa hata kidogo.

 

Hayo yamesemwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Mhe  Mwigulu  Lameki Nchemba wakati akiwahutubia raia hao wapya kwenye Makazi ya Katumba iliyoko katika  Halmashauri ya Nsimbo Wilayani Mpanda Mkoani Katavi ikiwa ni pamoja na kusisitiza kujiepusha na vitendo vya kubaguana.

 Akizungumzia kuhusu Uzalendo wa kuipenda nchi asisitiza na kuwataka raia hao kuepukana na tabia ya za chuki dhhidi ya nchi yako badala yake uzalendo uwe mbele kwanza kwa nchi.

Mapema Mhe  Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jeneral Mstaafu Raphael Muhuga amesema kuhusu suala la maeneo ya makazi kufutwa hati ya kuwa makazi, amesema eneo hilo haliwezi kufutwa hati ya kuitwa makazi  hadi taratibu za kuhakikisha wale wote wanaoishi katika makazi hayo ni raia wa Tanzania na hakuna mkimbizi katika maeneo hayo lakini kama kutakuwa bado wapo wakimbizi hati haiwezi kubadilishwa hadi taratibu zikamilike.

Pia amewasisitisitiza kutunza na kuhifadhi mazingira katika maeneo yao.

Mapema Mkuu wa Makazi ya Mishamo na Katumba Athman Igwe alieleza kuwa kata ya Katumba ni ya muda mrefu na ilianzishwa mwaka 1972 hadi kufika sasa kuna wakazi zaidi ya 78,000 lakini asilimia tisini na saba ni ya raia wapya hivyo bado kuna wakimbizi kwenye eneo hili.

Hivi karibuni kulikuwa na zoezi la kuhakiki wakimbizi kwa ajili ya kuwatafutia ufumbuzi wa kudumu zoezi lilianza tarehe 16 mwezi wa saba na limekamilika kwenye makazi haya mapya mwaka huu tarehe 3/8/ 2017 waliosajiliwa waliohakikiwa ni wakimbizi 11,329 kwa maana hiyo kuna kaya 5,134.

Pia Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba amewaasa watanzani wapya wanaoishi makazi ya Katumba na Mishamo Mkoani Katavi kuondoa fikra ya kuwa wao bado  ni wakimbizi badala yake wawe huru kwenda kuishi sehemu yeyote katika nchi maadamu wafuate taratibu na kuwasisitiza wale ambao hawajachukua vyeti vyao vya uraia wavichukue .

 Akihutubia kwenye mkutano wa Hadhara katika makazi ya Katumba na Mishamo Waziri Mwigulu ameeleza,na kuwasisitiza raia hao wapya na wale waliopatiwa vyeti vya uraia lakini hawataki kuchukua vyeti vyao waamue moja ama wachukue au waondoke kurudi kwao kwa kuwa kulikuwa hakuna haja ya kuomba uraia huo kama walikuwa hawautaki.

  Akizungumzia kuhama kutoka sehemu moja hadi nyingine katika nchi hii amesema ni jambo jema lakini amewaomba wasibadili majina yao bila kufuata utaratibu

Meja Jeneral Mstaafu Raphael Muhuga amewaasa kutunza mazingira pamoja na kusisitiza suala la kujitokeza kujiandisha kwa wale ambao hawakuandikishwa.

 Mapema Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Katavi Saidi Mselem amemweleza Waziri  wa Mambo ya Ndani ya Nchi kuwa wananchi wa Mishamo na Katumba wanakabiliwa na changamoto mbalimbali katika maeneo hayo kwa kuwa wako watanzania wapya na wale walioandikishwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved