• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

Historia

1.0 UTANGULIZI

1.1 Historia ya Mkoa

Mkoa wa Katavi una  ukubwa wa kilomita za mraba 47,527 na ulitangazwa rasmi tarehe 01 Marchi, 2012 kwa uamuzi wa serikali wa kuanzisha Mikoa minne mipya  ambayo ni (Katavi, Njombe, Simiyu na Geita) kwa lengo la kusogeza huduma za ki-utawala na Ki-uchumi kwa wananchi wake na ulizinduliwa rasmi tarehe 25/11/2012 na Mheshimiwa Gharib Bilal, Makamu wa Rais mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mujibu wa Amri ya Serikali ya maeneo ya kiutawala ya mwaka 2019, Mkoa wa Katavi una maeneo ya Kiutawala yafuatayo:-

S/N

WILAYA

HALMASHAURI

TARAFA

KATA

VIJIJI

VITONGOJI

MITAA

JIMBO

01

Mpanda
MPANDA MC

2 -Kashaulili na Misunkumilo.

15

14

81

43

MPANDA MJINI


NSIMBO DC

2-Nsimbo na Ndurumo

12

59

272

-

NSIMBO

02

Tanganyika
MPANDA DC

3-Karema, Kabungu na Mwese.

16

55

328

-

MPANDA VIJIJINI

04

Mlele
MLELE DC

1-Inyonga

6

18

85

-

KATAVI

05


MPIMBWE DC

2-Mpimbwe na Mamba

9

31

165

-

KAVUU

JUMLA

 

10

58

177

931

43

5

1.2 Mipaka ya Mkoa na Mahali Ulipo

Mkoa upo Magharibi mwa Tanzania kati ya Latitude 40 na 80 kusini mwa msitari wa Ikweta na Longitude 300 hadi 330 Mashariki mwa msitari wa Greenwich. Mipaka yake ni kama ifuatavyo:

  • Kaskazini unapakana na Wilaya za Urambo na Kaliua (Tabora)
  • Mashariki unapakana na Wilaya ya Sikonge (Tabora)
  • Kaskazini Mashariki unapakana na Wilaya ya Chunya (Mbeya)
  • Kusini unapakana na Wilaya ya Nkansi Nkansi (Rukwa)
  • Kusini Mashariki unapakana na Wilaya ya Sumbawanga (Rukwa)
  • Magharibi unapakana na Nchi ya Jamhuri ya Kidemorasia ya Kongo.
  • Kaskazini Magharibi unapakana na Mkoa wa Kigoma

1.3 Idadi ya Watu 

Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012, Mkoa una jumla ya wakazi 564,604, kati ya hao wanawake 289,817 na wanaume 274,787. Wastani kwa kaya moja ni watu 6 na uwiano wa kijinsia ni asilimia 98. Aidha, ongezeko la idadi ya watu ni asilimia 3.2 kwa mwaka. Mwaka 2016 Mkoa unakadiriwa kuwa na jumla ya watu 649,837 wanawake 327,934 na wanaume 321,903. Katika idadi hiyo kundi la nguvukazi ambao ni watu wenye umri wa miaka kati ya 15 na 64 wako 297,248.

1.4 Hali ya Kijiografia

Mkoa upo kati ya wastani wa mita 1000 hadi 2500 kutoka usawa wa bahari. Hali ya joto I kati ya nyuzi 130c ma 160c miezi ya Juni na Julai na nyuzi 260c hadi 300c miezi ya Septemba hadi Novemba. Kwa wastani, hupata mvua kati ya mm 700 hadi mm 1300 zinazonyesha kati ya Novemba na April. Mkoa umegawanyika katika kanda 4 za hali ya hewa ambazo ni ukanda wa bonde la ziwa Rukwa, Nyanda za uoto wa miombo ya Katumba-Inyonga, Miinuko ya Mwese na Mwambao wa ziwa Tanganyika.

Jedwali 1: Kuonesha Kanda, Eneo, Mwinuko, Kiwango cha Mvua na Shughuli za Kiuchumi.


Kanda
Eneo
Mwinuko
Udongo na kiwango cha mvua
Shughuli za Kiuchumi
Uwanda wa Katumba
Tarafa ya Nsimbo
1000-1500m
Udongo-udongo tifutifu unaopitisha maji kirahisi Mvua – 92mm-1000mm
1. Kilimo
Mahindi, Mihogo, Tumbaku , Maharage, Karanga, Alizeti & Miwa
2. Mifugo
Ng’ombe, Kondoo, Mbuzi, Kuku.
Nyanda za Mwese
Tarafa ya Mwese
1100-2500m
Udongo- udongo kichanga (Hilly)
Mvua- 100 -1100
1. Kilimo
Mahindi, Mihogo, Maharage, Ndizi, Kahawa, Viazi mviringo
2. Mifugo
Ng’ombe, Kondoo,Mbuzi,Kuku (poultry)
3. Nyinginezo: ufugaji nyuki
Bonde la Karema
Tarafa ya Karema
1000-1300m
Udongo – Udongo wa kichanga
Mvua
kiasi cha 1200mm.
1. Kilimo
Mahindi, Mhogo na Mpunga
2. Mifugo
Ng’ombe, Mbuzi, Kondoo, Kuku
3. Mengineyo
Uvuvi & Mbao
Bonde la ziwa Rukwa
Mpimbwe
Mwinuko unaanzia 1000-1100m upande wa kaskazini na 800 – 900 ufukweni wa Ziwa Rukwa.
Udongo- Udongo wa kichanga unaopitisha maji kidogo
Mvua – inanyesha kuelekea kusini kwa kiasi cha 1250 mm kwa mwaka hadi 840 mm-970mm chini ya miinuko ya Lyambalyamfipa .
1. Kilimo,
Mahindi, Mpunga, Matunda, (Horticulture), Mhogo, Ulezi, Mtama.
2. Mifugo
Ng’ombe, Mbuzi, Kondoo & Kuku
Nyingineyo
Uvuvi & Mbao
Ziwa Tanganyika
Karema
770-1300
Udongo – Kichanga unaopitisha maji.
Mvua
950-1200mm
1.Kilimo
Mahindi, Mhogo, Michikichi, Mpunga
2. Mifugo
Ng’ombe, Mbuzi na kondoo
3. shughuli Nyingineyo
Uvuvi



Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC KATAVI AHADI MAZINGIRA RAFIKI KWA WAWEKEZAJI

    March 09, 2023
  • RC KATAVI AWATAKA WANAWAKE KUSAMBAZA MAADILI MEMA KATIKA JAMII

    March 08, 2023
  • RC KATAVI ATOA POLE KWA WANANCHI WALIOGUSWA NA MSIBA WA AJALI YA BASI

    March 07, 2023
  • UKATILI KWA WATOTO HAUKUBALIKI KWA MWENYEZI MUNGU

    March 05, 2023
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • MWENGE BLOG-KATAVI
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved