• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

MAAFISA MAENDELEO YA JAMII KATAVI WAPEWA NGUVU MPYA KUFUNGUA FURSA ZA ZABUNI KWA MAKUNDI MAALUM.

Posted on: November 27th, 2025

Serikali kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) imewajengea uwezo maafisa maendeleo ya jamii ili waendelee kuwa daraja muhimu la kuwasaidia vijana, wanawake, wazee na watu wenye ulemavu kuzipata fursa za zabuni zilizotengwa kwa ajili yao.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo yaliyotolewa na PPRA kwa maafisa maendeleo ya jamii na maafisa ununuzi wa halmashauri zote za Mkoa wa Katavi, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa huo, Bw. Florence Chrisant, amesema ni jukumu la watendaji hao kuwajengea uwezo wanufaika ili waweze kuingia kwenye ushindani wa zabuni zinazotolewa na serikali.


Bw. Chrisant amesema kuwa vijana, wanawake, wazee na watu wenye ulemavu wanapaswa kujengewa uwezo ili kunufaika na asilimia 30 ya bajeti ya tenda za Serikali, ambayo mwaka huu wametengewa bajeti ya zaidi ya Shilingi Trilioni Tano. Aidha, amewataka maafisa hao kutumia vyema elimu waliyopewa na PPRA kuhakikisha wanatoa elimu zaidi kuwaandaa na kuwawezesha wahusika ili waweze kuitumia fursa hiyo muhimu inayotolewa na serikali yenye lengo la kuwainua kiuchumi.


"Serikali imewekeza nguvu kubwa kuhakikisha makundi maalum yanashiriki kikamilifu kwenye zabuni za umma, na ninyi ndiyo daraja lao. Nataka muende mkatekeleze haya kwa vitendo, muwafikie walengwa katika maeneo yenu na kuhakikisha fursa hizi haziishii kwenye makaratasi bali zinawafikia wananchi kwa uhalisia.” Amesema Bw. Chrisant


Nao maafisa maendeleo ya jamii wakitoa shukrani zao, wamesema mafunzo hayo yamewaongeza uelewa mpana kuhusu taratibu za ununuzi wa umma na namna ya kuwafikia wanufaika kwa ufanisi. Wameahidi kuyatumia mafunzo hayo kwa vitendo kwa kuhakikisha wanawafikia vijana, wanawake, wazee na watu wenye ulemavu katika maeneo yote ya mkoa, kuwapa elimu sahihi kuhusu ushiriki wa zabuni pamoja na kuwawezesha kujiandaa kushindana katika tenda za serikali.


Aidha, wamesisitiza kuwa wataendelea kuwa daraja la taarifa, ushauri na uhamasishaji kwa makundi maalum ili kuhakikisha wanaendelea kunufaika na uwekezaji mkubwa unaofanywa na serikali katika kuboresha uchumi wa wananchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • RATIBA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI - MWAKA 2025 April 28, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA SEKTA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI MKOA WA KATAVI August 27, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA SEKTA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI MKOA WA KATAVI August 27, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII KATAVI WAPEWA NGUVU MPYA KUFUNGUA FURSA ZA ZABUNI KWA MAKUNDI MAALUM.

    November 27, 2025
  • ELIMU JUMUISHI NA MALEZI BORA YA MTOTO YAJADILIWA KATIKA KIKAO CHA TATHMINI MKOA WA KATAVI

    October 08, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAFUNGUA NYUMBA YA WATUMISHI (2 KWA 1) KATA YA ISANJANDUGU.

    September 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI DARAJA LA MAWE KIGAMBONI.

    September 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved