• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

Waziri Mkuu Mhe.Kasim Majaliwa kufanya Ziara ya Siku 3 Mkoani Katavi

Posted on: December 10th, 2022

Pichani:Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Hoza Mrindoko alipotoa Taarifa ya ujio wa  Ugeni wa Mhe.Waziri Mkuu Kasim Majaliwa kwa  Waandishi wa Habari(Hawako pichani) Wilayani Mlele katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo 10 Disemba 2022.

Na:OMM -Mkoa 

Waziri Mkuu Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kasim Majaliwa Majaliwa atafanya Ziara ya siku 3 Mkoani Katavi, Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Hoza Mrindoko ameeleza.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Wilayani Mlele Mhe.Mrindoko ameeleza kuwa Mhe.Waziri Mkuu Kasim Majaliwa atawasili Mkoani Katavi siku ya Jumatatu Tarehe 12 Desemba 2022 ambapo atapokelewa na Viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali katika Uwanja wa Ndege wa Mpanda.

Akiwa Mkoani Katavi Mhe.Waziri Mkuu atakagua,kuzindua na kuweka Mawe ya Msingi Miradi mbalimbali ya maendeleo ambapo pia atasalimiana na Wananchi,pamoja na kuzungumza na Watumishi wa Umma wa  Mkoa wa Katavi.

Siku ya Tarehe 12 Disemba, 2022 baada ya kuwasili Mhe.Waziri Mkuu Kasim Majaliwa Majaliwa (Mb) ataelekea Wilayani Tanganyika kwa ajili ya kukagua na kuzindua miradi mbalimbali ya Maendeleo.

Akiwa Wilayani Tanganyika Mhe.Waziri Mkuu atazindua mradi wa Maji katika Kijiji cha Vikonge kilichopo Kata ya Tongwe na baada ya hapo ataelekea katika Kata ya Sibwesa kwa ajili ya kuweka Jiwe la Msingi Kituo cha Afya Sibwesa.

Baada ya hapo Mhe.Waziri Mkuu ataelekea Kata ya Kasekese kwa ajili ya kuweka Jiwe la Msingi katika Zahanati ya Kagunga na Madarasa Mawili.

Siku ya Tarehe 13 Disemba, 2022 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kasim Majaliwa Majaliwa (Mb) ataweka Jiwe la Msingi Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa  wa Katavi na kisha kuelekea Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo katika eneo la  Kabatini kwa ajili ya kutembelea Shamba la Korosho na Mahindi.

Baada ya hapo Mhe.Waziri Mkuu ataelekea Nsimbo Senta ambapo atakagua na kuzindua Kiwanda cha Maziwa cha MMS.

Baada ya hapo Mhe.Waziri Mkuu ataelekea Rungwa Manispaa ya Mpanda kutembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi, na kisha atazungumza na Watumishi wa Umma wa Mkoa wa Katavi katika Ukumbi wa Mpanda Social.

Aidha Siku ya Tarehe 14 Disemba 2022 Mhe Mrindoko ameeleza kuwa Mhe.Waziri Mkuu ataelekea Wilayani Mlele katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe kutembelea Kituo cha Afya Majimoto kilichijengwa kwa fedha za tozo pamoja na kuzindua matumizi ya Kituo hicho.

Akiwa Mpimbwe Mhe.Waziri Mkuu atahitimisha ziara yake kwa kufungua na kukagua Ujenzi wa Madarasa 13 ya Shule ya Sekondari Majimoto pamoja na kusalimia Wananchi wa Majimoto.

Mhe Mrindoko ametoa wito kwa Wananchi wote kujitokeza kwa wingi katika mapokezi ya ugeni huo mkubwa wa Kitaifa wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Amewataka Viongozi wa ngazi zote kujipanga vyema pamoja na kuhamasisha Wananchi kujitokeza kwa wingi kumpokea Mhe.Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved