Ikiwa ni takribani mwezi 1 tangu Mheshimiwa Naibu Waziri wa Tamisemi(elimu) Mheshimiwa Reuben Nhamanilo Kwagilwa azielekeze Halmashauri nyinginezo nchini kufika Halmashauri ya wilaya ya Mlele kujifunza namna bora ya utendaji kazi, wataalamu wa sekta ya elimu kutoka visiwani Zanzibar, wachangamkia fursa hiyo kwa kufika katika Halmashauri ya wilaya ya Mlele, lengo likiwa kujifunza kutoka kwa wataalamu wa Halmashauri hiyo kuhusu mbinu bora za elimu,utendaji kazi na kuhusu fursa mbalimbali zinazopatikana Halmashauri ya wilaya ya Mlele .

Wataalamu hao wamepata fursa ya kujifunza mambo mbalimbali vilevile wakapata fursa ya kutembelea shule ya sekondari ya amali_ ya Mgombe ambapo wamejifunza jinsi inavyoendesha huduma zake, sambamba na hilo wakapanda miti shuleni hapo ikiwa ni ishara ya kuunga mkono kauli mbiu ya " Uzalendo ni kutunza manzingira shiriki kupanda miti"

Aidha wataalamu hao wameipongeza Halmashauri ya wilaya ya Mlele kwa kazi nzuri inayofanya hali ambayo imewavutia wataalamu hao kuja kujifunza pia wakashukuru uongozi mzima wa Halmashauri hiyo kwa mapokezi mazuri uliowapatia .
Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Mlele Mheshimiwa Majid Mwanga kwa kushirikiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mlele Bi Siglinda Mdemu wamefurahishwa na ugeni huo hivyo wakawazawadia wataalamu hao Asali bora zaidi inayopatikana Halmashauri ya wilaya ya Mlele pekee vile vile wakatoa wito kwa wataalamu wengine kutoka maeneo mbalimbali kufika Mlele kujifunza fursa zilizopo.


Mpanda-Katavi (Mkoani Area)
Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi
simu: 025-2957108
Mobile:
Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz
Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved