• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

MHE. WAZIRI DKT. HOMERA ASISITIZA HUDUMA ZA KISHERIA NA UWAJIBIKAJI, VIONGOZI MKOA WA KATAVI WAPONGEZWA

Posted on: February 11th, 2026

Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera, leo Febuari 11, 2025, amewasili mkoani Katavi kwa ziara ya kikazi inayolenga kujenga uwezo wa viongozi wa umma na wadau wa sekta ya sheria.

Mhe. Dkt. Homera amepokelewa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi na mwenyeji wake, Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko, kabla ya kuanza rasmi ratiba ya mkutano wa kikazi unaohusisha mikoa ya Ukanda wa Magharibi na Nyanda za Juu Kusini.


Akiwa mkoani Katavi, atashiriki mkutano wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) pamoja na wajumbe wa Bodi za Wadhamini kutoka mikoa ya Katavi, Rukwa, Kigoma, Songwe, Mbeya na Tabora, wenye lengo la kuimarisha usimamizi na uwajibikaji wa bodi hizo.

Siku ya pili ya mkutano itawahusisha Maafisa Tarafa, Makatibu Tawala wa Wilaya na Wakuu wa Wilaya kwa lengo la kuwajengea uwezo katika kushughulikia masuala ya kisheria yanayowagusa wananchi, ikiwemo migogoro ya ardhi, ndoa na familia.

Mhe. Dkt. Homera amesema Wizara inaendelea kuboresha huduma za kisheria kwa kujenga na kukarabati mahakama za mwanzo ili kusogeza huduma karibu na wananchi.


“Serikali imejipanga kuhakikisha huduma za kisheria zinapatikana kwa urahisi na kwa kuzingatia misingi ya haki. Hatuwezi kufikia maendeleo bila kuimarisha uwajibikaji,” amesema.


Amesema wizara kwa kushirikiana na RITA imeweka utaratibu wa kutoa vyeti vya kuzaliwa ndani ya saa 48 baada ya kukamilika kwa usajili.


Aidha, Mhe. Dkt. Homera amepongeza uongozi wa Mkoa wa Katavi kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo, akieleza kuwa hatua hiyo imechangia kuimarika kwa huduma kwa wananchi na kuvutia uwekezaji.


Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko, amesema mkutano huo utawasaidia viongozi wa wilaya na tarafa kupata uelewa wa kina katika utatuzi wa migogoro inayowakabili wananchi.

Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA, Bw. Frank Kanyusi, amesema viongozi wa Wilaya ndiyo wanaokutana moja kwa moja na changamoto za wananchi, hivyo mafunzo hayo yataongeza ufanisi katika utoaji wa maamuzi kwa kuzingatia sheria.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • RATIBA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI - MWAKA 2025 April 28, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA SEKTA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI MKOA WA KATAVI August 27, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA SEKTA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI MKOA WA KATAVI August 27, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATAALAMU WA ELIMU KUTOKA ZANZIBAR WAVIKA H/W YA MLELE KUJIFUNZA.

    February 05, 2026
  • TIMU YA WATAALAMU WA ELIMU KUTOKA ZANZIBAR YAFANYA ZIARA YA MAFUNZO H/W YA MPIMBWE.

    February 04, 2026
  • MHE. WAZIRI DKT. HOMERA ASISITIZA HUDUMA ZA KISHERIA NA UWAJIBIKAJI, VIONGOZI MKOA WA KATAVI WAPONGEZWA

    February 11, 2026
  • RAS MSOVELA AWATAKA WATUMISHI WA UMMA WILAYA YA TANGANYIKA KUWA MFANO WA KUIGWA, KUJENGA HUDUMA BORA, UWAZI NA UWAJIBIKAJI.

    December 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved