• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

Wananchi Tanganyika walalamika kutozwa ushuru chini ya tani Moja, RC Katavi awataka Viongozi kujitathmini.

Posted on: August 12th, 2022

Pichani:Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Majalila Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika alipofanya ziara katika Halmashauri hiyo 11 Agosti 2022


Baadhi ya Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Wilayani Mpanda Mkoani Katavi wameeleza mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko kuwa licha ya Serikali kufuta ushuru chini ya tani moja bado watoza ushuru ndani ya Halmashauri hiyo wameendelea kuwatoza wakulima wanaosafirisha mazao yao chini ya tani moja.

John Madege Mkazi wa Kijiji cha Majalila Wilayani Tanganyika ameeleza kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakisumbuliwa na kutozwa ushuru wa mazao yao chini  tani moja licha ya makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Philip Isdor Mpango kukekemea vikali tabia hiyo katika ziara yake Wilayani Tanganyika siku chache zilizopita.

Bw.Madege ameulalamikia utaratibu wa utoaji wa vibali vya kusafirisha ushuru chini ya tani moja katika ofisi za watendaji wa kata ndani ya Halmashauri hiyo kuwa ni changamoto kutokana na kukumbana na usumbufu Mkubwa.

Kufuatia changamoto hiyo Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko amewaelekeza Mkuu wa Wilaya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo kuhakikisha kuwa wanakomesha tabia hiyo inayofaanywa na baadhi ya watumishi wasiokuwa waaminifu ambao wamekuwa wakikiuka maagizo na maelekezo ya viongozi wa ngazi za juu.

Amesema kuwa kitendo cha Wananchi kuendelea kutozwa ushuru chini ya tani moja ni kiashiria kuwa viongozi wa Halmashauri hiyo  wameshindwa kusimamia kikamilifu maagizo ya viongozi wa ngazi za juu na kwamba wanapaswa kujitathmini.

Amewaelekeza Viongozi wa Halmashauri kuhakikisha kuwa Wananchi ambao wanasafirisha mazao chini ya tani moja wasitozwe ushuru kama ilivyoelekezwa na viongozi mbalimbali wa serikali na kwamba hatosita kuchukua hatua kwa kiongozi yeyote iwapo itathibitika kusababisha usumbufu huo kwa wananchi.

Kwa upande wake kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Bw.Desu Luziga ameeleza kuwa Halmashauri imetoa utaratibu wa kupata vibali kwa wakulima wanaosafirisha mazao chini ya tani moja lakini Wakulima wamekuwa na muitikio mdogo kukata vibali hivyo vinavyotolewa katika Ofisi ya Mtendaji wa Kata.

Ameongeza kuwa Halmashauri imekuwa ikipambana na baadhi ya wakulima wasio waaminifu wanaokwepa ushuru kwa kutumia mgongo wa wakulima wadogo wadogo ambapo wafanyabiashara wakubwa wamekuwa wakiwatumia wakulima wadogo na vijana wa bodaboda kusafirisha mazao chini ya tani moja ili kukwepa ushuru.

Bw.Luziga ameeleza kuwa pindi Watoza ushuru wanapobaini utoroshwaji wa mazao wa namna hiyo wamekuwa wakijizatiti kudhibiti hali hiyo ili kudhibiti mapato ya halmashauri ambapo amewataka wakulima wadogo wadogo kuhakikisha kuwa wanapata vibali vya kusafirisha mazao hayo katika ofisi za watendaji wa Kata ili kupuka usumbufu magetini.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • KATAVI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI.

    May 21, 2025
  • BASATA YAWAPIGA MSASA MAAFISA UTAMADUNI NA BIASHARA KATAVI MFUMO WA AMIS NA TAUSI

    May 20, 2025
  • KATAVI KUANZA KUTUMIA UMEME WA GRID YA TAIFA MEI 20,2025.

    May 15, 2025
  • KATAVI YAZIDI KUNG'ARA UUZAJI WA KABONI

    May 13, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved