• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

UZINDUZI WA MIKOPO YA 10% KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU

Posted on: December 10th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mhe. Jamila Yusuph amemuakilisha Mhe. Mwanamvua Mrindoko Mkuu wa Mkoa wa Katavi Katika
Uzinduzi Rasmi wa zoezi la  utoaji wa Mikopo  ya Asilimia 10% kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye ulemavu, ambazo ni Fedha za Mapato ya ndani ya Halmashauri na kutoa Hundi ya Mfano yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.3.

"Natoa pongezi kwa Vikundi vyote , Fedha hizo  mkazitumie kulingana na Malengo mliyojiwekea. Mkoa wa Katavi unaenda kutoa Fedha Bilioni 2.3 kwa vikundi vitatu, Wanawake , Vijana na Watu wenye Ulemavu, mkazitumie vizuri Ili mkatimize Malengo yenu". Amesema Mhe. Jamila Yusuph.

Mhe. Jamila amewasihi wote walioomba na watakaopata Mikopo hiyo kuzingatia kanuni, taratibu na Sheria za Mikopo ili ikatoe matokeo chanya katika shughuli wanazoenda kuzifanya na kutimiza azma ya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha vikundi mbalimbali  vya wanawake, Vijana na Watu wenye ulemavu vinajikwamua kiuchumi.

Akizungumza mala baada ya Uzinduzi huo Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mpanda, Mhe. Haidari Sumry amesema kuwa vikundi vyote vilivyopewa mikopo vifanye kazi iliyokusudiwa ili viweze kunufaika na kurejesha mikopo hiyo kwa wakati, ili kundi lingine liweze kunufaika na mikopo hii.

"Serikali imeamua kurejesha mikopo hii ya asilimia 10 ya Vijana, Wanawake na watu wenye Ulemavu, ikiwa na dhamira ya kutoa ajira na kuboresha uchumi wa mtu mmoja mmoja na uchumi wa Mkoa wetu kwa ujumla". Amesema.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kikundi cha Boda Boda Wilaya ya Mlele Bwana Joshua Gabriel Mosses amesema, "Tunapenda kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe .Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuyakumbuka makundi yote na kuyawewezesha kupata mikopo hii kwa awamu nyingine toka isitishwe.

"sisi kama wana kikundi tutautumia vizuri mkopo huu na kuhakikisha tunarejesha kwa wakati ili wanufaika wengine wapate fursa hii". Amesema.

Uzinduzi huo umefanyika leo Jumanne tarehe 10 Desemba katika Ukumbi wa Mpanda Social Hall uliopo Manispaa ya Mpanda.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved