• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

RC MRINDOKO AZUNGUMZA NA BARAZA LA WAZEE KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

Posted on: July 28th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko, leo Julai 28, 2025 amekutana na Mabaraza ya Wazee kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Katavi kwa lengo la kuimarisha maandalizi ya Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.

Kikao hicho kimefanyika ikiwa ni sehemu ya mkakati wa Serikali ya Mkoa kuhakikisha uchaguzi unafanyika katika mazingira ya amani, mshikamano, na kuheshimu misingi ya haki, usawa na demokrasia. Wazee wamehusishwa kutokana na nafasi yao muhimu katika jamii kama wahifadhi wa mila, washauri wa kijamii, na daraja kati ya Serikali na wananchi.

Katika mkutano huo, Mkuu wa Mkoa amewashukuru Wazee kwa namna ambavyo wameendelea kuwa sehemu ya ustawi wa mkoa, hususan katika kushiriki kwenye masuala ya kijamii na kutoa ushauri kwa Serikali katika nyanja mbalimbali za maendeleo.

Aidha, RC Mrindoko amewaomba Wazee kuendelea kuhubiri amani, mshikamano na upendo katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu, huku akiwasihi kuwa mstari wa mbele katika kuzuia na kuripoti viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani vinavyoweza kujitokeza katika maeneo yao.

Pamoja na hilo, Mkuu wa Mkoa amewataka Wazee kuwa walimu kwa wagombea wa nafasi mbalimbali pamoja na wananchi, kwa kuwaelimisha kuhusu umuhimu wa kushiriki uchaguzi kwa kufuata sheria, kuepuka rushwa, uchochezi, lugha za matusi, na vitendo vyote vinavyokinzana na maadili ya kitanzania.


Sambamba na hayo, Wazee wametoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa uongozi mahiri, utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya maendeleo, na dhamira yake ya kuimarisha ustawi wa wananchi kupitia sera na mipango ya kitaifa.


Mkutano huo umehitimishwa kwa wito wa Mkuu wa Mkoa kwa Wazee kushiriki kikamilifu katika zoezi la uchaguzi mkuu na kuendelea kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi hilo muhimu kwa mustakabali wa Taifa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZUNGUMZA NA BARAZA LA WAZEE KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

    July 28, 2025
  • ZIARA YA WAZIRI WA MAJI, MRADI WA MAJI WA MIJI 28 WILAYA YA MPANDA.

    July 24, 2025
  • SEPTEMBA 2025, MWISHO WA MATUMIZI YA MKAA NA KUNI KWENYE TAASISI ZINAZO HUDUMIA WATU ZAIDI YA 100. HUDUMIA

    July 23, 2025
  • KATAVI YAANZA KUYABAINISHA MAENEO HATARISHI YANAYOCHOCHEA MAGONJWA YA MLIPUKO.

    July 22, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved