• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

Posted on: May 5th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko, ameongoza hafla ya uzinduzi wa Juma la Elimu Kitaifa (GAWE 2025) kwa kutoa wito kwa wadau wa elimu kuendeleza ushirikiano na Serikali katika kuleta mabadiliko chanya kwenye sekta ya elimu nchini.

Katika hotuba yake, RC Mrindoko amesisitiza dhamira ya Serikali ya kuimarisha ushirikiano na Mtandao wa Elimu Tanzania kama sehemu ya juhudi za kuboresha ubora wa elimu, hususan kwa kuhakikisha elimu inakuwa jumuishi na yenye tija kwa kila mtoto wa Kitanzania.

Akiweka mkazo kwenye changamoto ya mimba na ndoa za utotoni maarufu kama “Chagulaga”, Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa mila na desturi zisizofaa zinaendelea kuwa kikwazo kwa elimu ya watoto wa kike. Amewataka wazazi na jamii kwa ujumla kulinda haki ya mtoto wa kike kupata elimu bila vikwazo vya kijamii na kiutamaduni.

Vilevile, amesisitiza umuhimu wa familia na jamii kuhifadhi mavuno kwa mwaka mzima ili kupunguza changamoto ya utoro mashuleni unaotokana na uhaba wa chakula, hali ambayo huathiri utekelezaji wa mpango wa lishe mashuleni na maendeleo ya kitaaluma ya wanafunzi.


Kwa upande wake, Afisa Elimu wa Mkoa wa Katavi, Bi. Dafroza Ndalichako, amewasilisha taarifa ya hali ya elimu mkoani humo, akieleza kuwa hadi kufikia Machi 31, 2025, jumla ya wanafunzi 29,782 wameandikishwa katika elimu ya awali, ikiwa ni asilimia 77.5 ya lengo la kuandikisha watoto 37,796.

Aidha ameendelea kuhimiza ushirikiano thabiti kati ya Serikali na wadau wa elimu katika kutatua changamoto hizo na kuimarisha maendeleo ya elimu mkoani Katavi.

Naye Mwenyekiti wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bi. Faraja Nyarandu, ameeleza kuwa mfumo wa elimu nchini unapaswa kujengwa kwa misingi ya utu, usawa na ubora. Amehimiza kuondolewa kwa adhabu zisizofaa mashuleni na matumizi ya mbinu mbadala za malezi zenye kujenga mazingira rafiki kwa watoto kujifunza.


Aidha, amesisitiza umuhimu wa uwekezaji katika elimu ya ujuzi, lishe mashuleni, afya ya uzazi kwa vijana na miundombinu bora ili kuhakikisha kila mtoto wa Kitanzania anapata elimu bora, salama na jumuishi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved