• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

RC MRINDOKO AZIAGIZA HALMASHAURI ZOTE KATAVI KUSAMBAZA MBEGU BORA ZA UFUTA KWA WAKULIMA ILI KUONGEZA UZALISHAJI MSIMU UJAO.

Posted on: August 8th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko, ameziagiza Halmashauri zote za mkoa wa Katavi kuhakikisha zinapata mbegu bora za zao la ufuta na kuzisambaza kwa wakulima kwa wakati muafaka ili kuongeza uzalishaji msimu ujao. Amesema mbegu bora ni msingi wa kilimo chenye tija, na kuzitumia kunahakikisha wakulima wanapata mavuno mengi zaidi.

“Kwa kuwa masoko ya ufuta yameimarika kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani, fursa kwa wakulima ni kubwa zaidi kufanikisha uzalishaji bora na wenye tija. Halmashauri pia zitanufaika kwa mapato zaidi, ambayo yatawezesha kuendeleza huduma za kijamii na miundombinu,” amesema RC Mrindoko.

Pia, amewataka maafisa ugani kuwatembelea wakulima mara kwa mara na kuwapatia elimu ya mbinu bora za kilimo ili kuongeza uzalishaji na kuboresha tija. Amesisitiza kuwa elimu endelevu ni muhimu kwa wakulima kufanikisha kilimo cha kisasa.

RC Mrindoko ametoa kauli hiyo alipotembelea banda la Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika kwenye maonesho ya Nanenane 2025 yaliyohitimishwa leo katika Viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya. Aidha, amepongeza mafanikio ya mkoa wa Katavi msimu huu na kusema maonesho ya mwaka huu yameonesha maendeleo makubwa ikilinganishwa na misimu iliyopita.

Vilevile, amewataka wakulima kujisajili ili kunufaika na mbolea za ruzuku zinazotolewa kwa gharama nafuu, hatua ambayo ni sehemu ya mkakati wa serikali kusaidia kupunguza gharama za uzalishaji.

“Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha nyingi kwa ajili ya malipo ya mbolea za ruzuku, hivyo wakulima wanatakiwa kunufaika kwa kujisajili mapema,” amesema RC Mrindoko.


Ameongeza kuwa ushirikiano wa karibu kati ya halmashauri, maafisa ugani na wakulima ni muhimu ili kuhakikisha mkulima yeyote anapata msaada unaohitajika kwa wakati unaofaa.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • BENKI YA CRDB YATOA MSAADA WA MADAWATI SHULE YA WASICHANA KATAVI

    August 12, 2025
  • RC MRINDOKO AZIAGIZA HALMASHAURI ZOTE KATAVI KUSAMBAZA MBEGU BORA ZA UFUTA KWA WAKULIMA ILI KUONGEZA UZALISHAJI MSIMU UJAO.

    August 08, 2025
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA MPANDA YANG’ARA NANENANE 2025, YASHIKA NAFASI YA TATU.

    August 08, 2025
  • MRINDOKO AHIMIZA UBUNIFU NA ABAINISHA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOANI KATAVI.

    August 06, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved