Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

RC MRINDOKO ATOA WITO KWA VIONGOZI KUHAMASISHA MATUMIZI YA CHAKULA CHENYE VIRUTUBISHI ILI KUTOKOMEZA UDUMAVU.

Posted on: June 10th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko, amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri pamoja na Wakuu wa Wilaya kuhakikisha jamii inahamasishwa kutumia vyakula vilivyorutubishwa ili kukabiliana na changamoto ya udumavu na kuboresha afya ya wananchi.

Akiwaongoza wadau wa chakula katika kikao kazi kilichofanyika leo katika ofisi yake kwa lengo la kuwajengea uelewa kuhusu urutubishaji wa chakula, RC Mrindoko amesisitiza umuhimu wa kutoa elimu kwa jamii juu ya lishe bora na virutubishi muhimu, sambamba na kuondoa dhana potofu kuhusu vyakula vilivyorutubishwa.

Pamoja na kuwa mkoa wa Katavi ni miongoni mwa wazalishaji wakuu wa mazao ya chakula nchini, hali ya lishe bado hairidhishi. Mkoa unaendelea kuchukua hatua madhubuti, ikiwa ni pamoja na kuongeza virutubishi kwenye chakula kupitia teknolojia ya usindikaji wa mazao. Katika hatua hiyo, Katavi imepokea mashine 20 mpya za usindikaji mazao kwa ajili ya kuongeza virutubishi kwenye vyakula, ambapo hadi sasa mashine 15 kati ya 359 zinazotumika kusaga unga zimeboreshwa kurutubisha chakula, sawa na asilimia 73 ya mashine zote.

Kaimu katibu tawala wa mkoa wa Katavi, Bw. Nehemia James, amebainisha kuwa mkoa unaendelea kutekeleza kampeni ya lishe kupitia mpango harakishi wa kupunguza udumavu. Mpango huo unajumuisha ushirikiano wa sekta mbalimbali na jitihada za uelimishaji kwa jamii nzima.

Wakati huohuo, Peter Kaja kutoka Wizara ya Afya ameeleza kuwa sehemu kubwa ya jamii inakula vyakula vilivyokobolewa au vya mizizi ambavyo kwa kawaida vina kiwango kidogo cha virutubishi. Amefafanua kuwa ukoboaji wa nafaka hupoteza zaidi ya asilimia 75 ya virutubishi, kwani vitamini na madini vingi hupatikana kwenye pumba na kiini cha nafaka.

Kikao hicho kimehitimishwa kwa kauli ya pamoja inayotaka wadau wote kuongeza kasi ya utoaji elimu ya lishe, kutumia teknolojia za kurutubisha chakula, na kushirikiana katika kuleta mabadiliko chanya ya kiafya kwa jamii ya Mkoa wa Katavi.





Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • BARAZA MAALUM LA MADIWANI TANGANYIKA LAJADILI TAARIFA YA CAG, WATUMISHI WATAKIWA KUFUATA SHERIA.

    June 17, 2025
  • RAS MSOVELA AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA NSIMBO KWA KUTEKELEZA MAAGIZO YA KAMATI YA BUNGE.

    June 19, 2025
  • MAADHIMISHO SIKU YA MTOTO AFRIKA, CHAGULAGA BADO NI KILIO KWA WASICHANA KATAVI.

    June 16, 2025
  • RC MRINDOKO ATOA WITO KWA VIONGOZI KUHAMASISHA MATUMIZI YA CHAKULA CHENYE VIRUTUBISHI ILI KUTOKOMEZA UDUMAVU.

    June 10, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved