• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

RC MRINDOKO ATOA MIPANGO YA MAENDELEO 2025 KWA WANANCHI WA KATAVI

Posted on: January 1st, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mheshimiwa Mwanamvua Mrindoko, leo Januari 1, 2025, amesema kuwa wananchi wa Katavi wanapaswa kusherehekea mwaka mpya kwa amani na utulivu.


Katika salamu zake, Mheshimiwa Mrindoko ametumia fursa hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa jitihada kubwa zilizotekelezwa ndani ya mkoa wa Katavi mwaka 2024 na mipango kabambe iliyopangwa kwa mwaka 2025 na kuendelea.


Amesema kuwa mkoa umejipanga kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi, ikiwa ni pamoja na kuboresha sekta za elimu, maji, barabara, na afya. Lengo kuu ni kuhakikisha huduma hizi zinapatikana kwa ubora na kuwafaidisha wananchi wote wa Katavi.


Mheshimiwa Mrindoko ameweka msisitizo wa kuongeza uzalishaji katika sekta zote za uchumi, hasa kilimo, ambacho kimebainishwa kuwa uti wa mgongo wa usalama wa chakula. Ameeleza kuwa suala la usalama wa chakula ni ajenda muhimu kwa Tanzania na dunia nzima, na hivyo litapewa kipaumbele.


Amesema mkoa utaendelea kuimarisha masoko kwa mazao ya kilimo, mifugo, nyuki, na misitu, ikiwa ni pamoja na masoko ya minada na kuboresha Bandari ya Karema. Kwa mujibu wa Mheshimiwa Mrindoko, hatua hizi zinalenga kuwasaidia wakulima na wafanyabiashara wa mkoa wa Katavi kupata faida zaidi kutoka kwenye juhudi zao.


Katika sekta ya michezo na sanaa, Mkuu  wa Mkoa amesema mkoa umeazimia kuibua vipaji vipya na kuendeleza sekta hiyo kwa kujenga miundombinu bora, ikiwa ni pamoja na kiwanja cha kisasa na timu ya mkoa itakayokuwa ikitangaza Katavi. Amesema juhudi hizi zinalenga kuimarisha maendeleo ya vijana na kutoa nafasi zaidi katika sekta ya burudani.


Aidha, Mheshimiwa Mrindoko amesema mkoa utaweka mkazo kwenye utunzaji wa mazingira, usafi, na upendezeshaji wa miji, akihimiza ushirikiano wa wananchi katika kuhakikisha Halmashauri zote za Katavi zinakuwa safi na zenye mvuto.


Ameeleza kuwa juhudi za kukuza utalii zitaharakishwa kwa kuhakikisha mbuga ya Katavi inatangazwa kikamilifu. Amesema mkoa umejipanga kuvutia wageni wa ndani na nje ya nchi ili kuchochea ukuaji wa uchumi katika sekta ya utalii.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved