• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

RC MRINDOKO AKEMEA WAKURUGENZI KUZALISHA MADENI MAPYA KWA WAZABUNI.

Posted on: May 22nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko, amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote mkoani hapa kuepuka kuanzisha madeni mapya kwa wazabuni, kwa kuwa Serikali hutenga fedha kamili kwa ajili ya utekelezaji wa miradi na hulipa madeni yaliyopo kwa kutumia bajeti iliyopangwa bila kuongeza madeni mengine mapya.

Agizo hilo amelitoa leo, Mei 22, 2025, katika kikao kazi kilichowakutanisha Mkuu wa Mkoa, wazabuni na wakuu wa taasisi mbalimbali, ambapo walijadili jitihada zinazofanywa na Serikali kushughulikia madeni ya wazabuni pamoja na changamoto wanazokutana nazo.


Amesema kuwa baadhi ya watumishi wasio waaminifu wamekuwa wakichelewesha kushughulikia madai ya wazabuni, hali inayosababisha ongezeko la madeni. Ameelekeza kuwa wazabuni wanapaswa kuhakikisha wanazingatia matumizi sahihi ya nyaraka za zabuni ili kuepuka mkanganyiko unaoweza kujitokeza wakati wa ulipaji.

“Tuna mkakati wa kulipa madeni yote ya wazabuni kupitia bajeti ya kipindi cha miaka mitatu. Tayari tumeanza kupunguza madeni tangu bajeti ya mwaka 2024/2025, na tunatarajia hadi kufikia mwaka 2026/2027 tutakuwa tumemaliza kulipa madeni yote,” amesema Mhe. Mrindoko.

Ameongeza kuwa kutokana na jitihada hizo, Serikali ya Mkoa imefanikiwa kupunguza jumla ya madeni ya wazabuni kutoka shilingi bilioni 2.38 hadi kufikia malipo ya shilingi milioni 755.16 kwa baadhi ya wazabuni.


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Mkoa wa Katavi, Bw. Amani Mahela, ametoa wito kwa wafanyabiashara kujiunga na chama chao ili kurahisisha ufuatiliaji wa madeni pamoja na upatikanaji wa taarifa sahihi kutoka kwa mamlaka husika.

“Taarifa nyingi kutoka serikalini huletwa katika ofisi zetu, lakini wafanyabiashara wengi hawazipati kwa sababu hatuna taarifa zao sahihi. Hivyo tunawasihi wajiunge na chama chetu ili tuweze kuwahudumia kwa ufanisi,” amesema Bw. Mahela.






Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AKEMEA WAKURUGENZI KUZALISHA MADENI MAPYA KWA WAZABUNI.

    May 22, 2025
  • KATAVI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI.

    May 21, 2025
  • BASATA YAWAPIGA MSASA MAAFISA UTAMADUNI NA BIASHARA KATAVI MFUMO WA AMIS NA TAUSI

    May 20, 2025
  • KATAVI KUANZA KUTUMIA UMEME WA GRID YA TAIFA MEI 20,2025.

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved