• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

Posted on: April 29th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko, ameihakikishia Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kuwa Mkoa wa Katavi haujawahi kuwa kikwazo katika utekelezaji wa shughuli yoyote iliyopangwa na Serikali, hivyo hata zoezi la uchaguzi mkoani humo linaendelea kuandaliwa kwa amani na utulivu.


RC Mrindoko ametoa kauli hiyo Aprili 29, 2025, wakati akiipokea na kuikaribisha Tume hiyo mkoani Katavi kwa ajili ya maandalizi ya zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

Aidha, Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa tayari Serikali ya Mkoa imeanza kutekeleza jukumu hilo kwa kutoa elimu kwa wananchi kuhusu uchaguzi na upigaji kura kupitia mikutano mbalimbali, na amewasihi wananchi kujitokeza kwa wingi katika vituo vitakavyotangazwa ili kusahihisha au kuhuisha taarifa zao.

“Tumejipanga kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani. Na kuanzia sasa, niseme tu kuwa ofisi yangu inatoa ushirikiano wa kutosha hadi pale uchaguzi utakapo kamilika,” amesisitiza Mheshimiwa Mrindoko.

Kwa upande wake, Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama Kuu Asina Omari, amesema kuwa Tume imejipanga kikamilifu kwa ajili ya maandalizi ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, ikiwemo kwa Mkoa wa Katavi.


Amefafanua kuwa uboreshaji huo unahusisha kuwaandikisha raia wa Tanzania waliotimiza umri wa miaka 18 na zaidi, au watakaotimiza umri huo kabla ya tarehe ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, pamoja na wale ambao hawajapoteza sifa kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi au sheria nyingine yoyote.


Zoezi hilo pia linahusisha wapiga kura waliobadili makazi kutoka vituo walivyojiandikisha awali, waliopoteza sifa, wenye taarifa zisizo sahihi pamoja na waliopoteza au kuharibu kadi zao za kupigia kura.


Aidha, Mwenyekiti wa Tume hiyo amemuomba Mkuu wa Mkoa kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha elimu kuhusu uboreshaji wa Daftari inawafikia wadau wote, akizingatia kuwa ana mtandao wa wasaidizi hadi katika ngazi za chini za utawala.


Zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa Mkoa wa Katavi linatarajiwa kuanza rasmi kuanzia Mei 1 hadi Mei 7, 2025.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • KATAVI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI.

    May 21, 2025
  • BASATA YAWAPIGA MSASA MAAFISA UTAMADUNI NA BIASHARA KATAVI MFUMO WA AMIS NA TAUSI

    May 20, 2025
  • KATAVI KUANZA KUTUMIA UMEME WA GRID YA TAIFA MEI 20,2025.

    May 15, 2025
  • KATAVI YAZIDI KUNG'ARA UUZAJI WA KABONI

    May 13, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved