• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

RC Katavi azindua mradi wa maji Isinde/Mtapenda akabidhi pikipiki, Awataka Wananchi kulinda miundmbonu ya Maji.

Posted on: August 13th, 2022

Pichani:Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko akikata utepe ishara ya kuzindua zoezi la ugawaji wa pikipiki zilizotolewa na RUWASA makao makuu kwa ajili ya jumuia za watumia maji 12 Agosti 2022.


Isinde Mtapenda

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko amewataka Wananchi Mkoani Katavi kuwa walinzi wa miundombinu ya Maji pamoja na vifaa mbalimbali vinavyosaidia kurahisisha upatikanaji wa huduma hiyo ili kuendelea kunufaika na miradi inayojengwa na Serikali kwa ajili yao.

Mhe.Mrindoko ametoa rai hiyo akiwa Isinde Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo katika hafla ya uzinduzi wa mradi wa maji wa Mtakuja/Songambele pamoja na tukio la kukabidhi piki piki 10 zilizotolewa na Wakala ya usambazaji maji na usafi wa mazingira Vijijini RUWASA Makao makuu zenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 32 kwa ajili ya usimamizi wa huduma za Maji katika ngazi ya Jamii.

 Mhe.Mkuu wa Mkoa amewataka Wananchi kuwa walinzi wa vyombo vya usafiri vilivyotolewa kuhakikisha kuwa vinatumika kwa shughuli iliyokusudiwa ya kusimamia shughuli za upatikanaji wa Maji katika ngazi ya Jamii.

Aidha Mhe.Mrindoko amemtaka Meneja wa RUWASA Mkoa wa Katavi kuhakikisha kuwa miradi yote ambayo haikuwa imekamilika katika kipindi cha mwaka wa fedha uliopita 2021/2022 pamoja na miradi ambayo utekelezaji wake unafanyika katika kipindi cha mwaka wa fedha 2022/2023 inakamilika kwa wakati ili wananchi waweze kuondokana na changamoto ya uhaba wa maji katika maeneo yao.

Kwa upande wake meneja wa RUWASA Mkoa wa Katavi Bw.Peter  Ngunula amesema Mkoa umepokea pikipiki hizo kutoka RUWASA makao makuu kwa ajili ya Wilaya tatu za Mlele,Tanganyika na Mpanda.

Akizungumzia kuhusu hali ya upatikanaji wa maji Mkoani Katavi Bw,Ngunula amesema hali ya upatikanaji wa maji Mkoani Katavi ni Asilimia 70 ambapo katika kipindi cha mwaka wa fedha uliopita 2021/2022 miradi iliyokuwa katika utekelezaji ilikuwa 41 yenye thamani ya Shilingi Bilioni 27. ambapo kwa mwaka huu wa fedha 2022/2023 ruwasa Mkoa wa Katavi unatekeleza miradi 4 yenye thamani ya shilingi Bilioni 4.19

Ngunula amesema kuwa kukamilika kwa miradi ya Maji inayotekelezwa kwa mwaka huu wa fedha 2022/2023 kutapelekea huduma ya maji kuwafikia watu wengi zaidi ambapo upatikanaji wa Maji unatarajiwa kuwa asilimia 88.

Kwa upande wao Diwani wa Kata ya Mtapenda Mhe.Eliezeli Fyula pamoja na Diwani wa Kata ya Kapalala Mhe.Lindila Matege kwa niaba ya Wananchi wameishukuru Serikali ambapo wameahidi kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha kuwa miundombinu ya Maji inatunza na kulindwa.

 

 



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved