• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

RC KATAVI AWATAKA WANANCHI KUDUMISHA AMANI

Posted on: April 7th, 2023

 

RC KATAVI AWATAKA WANANCHI KUDUMISHA AMANI


Amani ndiyo msingi mkubwa wa maendeleo duniani. Binadamu au taifa lolote duniani haliwezi kuwa na maendeleo yoyote yale bila kuwa na amani.

Amani huvutia wawekezaji, hujenga mazingira ya uzalishaji, huwawezesha watu kufanya shughuli mbali za kijamii na kiroho mfano kuabudu. Kumbe amani ni muhimu siyo tu katika kuwezesha maendeleo katika jamii bali katika kudumisha maendeleo endelevu.

Hakuna serikali duniani isiyopenda amani na utulivu kwa wananchi wake na mipaka yake. Daima serikali huwahimiza wananchi wake kuimarisha na kudumisha amani kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wenyewe na taifa kwa ujumla.

Serikali duniani zimeweka sheria, kanuni na taratibu ili kuhakikisha kuwa amani na utulivu vinadumishwa kwa wananchi na mipaka yake.

Tanzania ni miongoni mwa serikali duniani zilizojiwekea sheria, kanuni na taratibu kwa ajili ya kuhakikisha kuwa amani na utulivu vinadumu nchini na kwa wananchi wake.

Mkoani Katavi, kiongozi mkuu wa mkoa huo, Mhe. Mwanamvua Mrindoko anajitokeza mbele ya vyombo vya habari kuwapongeza wakristo wote mkoani kwake na taifa kwa ujumla kwa kuendesha mfungo wa kwaresma na kuingia katika sikukuu za pasaka kwa amani na utulivu mkubwa.

Mhe. Mrindoko anasema mkoa umeendelea kuwa salama, tulivu na shwari kutokana na ushirikiano mkubwa ambao wananchi wake wameutoa kwa vyombo vya dola katika kudumisha amani na utulivu.

Katika maadhimisho ya sikukuu za pasaka, kiongozi huyo anatoa maelekezo na tahadhari mbali mbali katika kipindi chote cha maadhimisho ya sikukuu na baada ya sikukuu hizo.

Mhe. Mrindoko anawaonya wananchi wote waliojipanga kufanya fujo na ghasia kwa wakristo wote watakao kuwa kwenye ibada kuwa wasithubutu kufanya hivyo kwa kuwa watajutia kupanga hivyo.

Amesema vyombo vya dola vimejipanga kuhakikisha kuwa usalama na utulivu vinaendelea kuwepo sehemu zote za ibada, majumbani na katika kumbi zote za starehe.

Mhe. Mrindoko amesema vyombo vya dola vitafanya doria na misako sehemu mbali mbali ili kuhakikisha kuwa amani inatamalaki katika mkoa wakati wote wa sikukuu na baada ya sikukuu

Kuhusu watoto na wanafunzi, Mhe Mrindoko amepiga marufuku kwa watoto au wanafunzi kwenda kwenye kumbi za starehe na badala yake wapelekwe kwenye maeneo ya wazi ambapo hakuna uwezekano wa kutokea ajali yoyote

Ameonya wazazi watakaokiuka agizo hilo, vyombo vya dola vitawachukulia hatua za kisheria ili kukomesha tabia hiyo

Pamoja na marufuku hiyo, kiongozi huyo amewatahadharisha wanaoendesha vyombo vya moto kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zote za usalama barabrani ili kuepusha ajali zisizo za lazima katika kipindi na baada ya sikukuu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved