Pichani Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko alipozungumza na Wananchi wa Majalila katika uwanja wa shule ya Msingi Majalalila Wilayani Tanganyika 11 Agosrti 2022
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko amemuagiza kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi kufuatilia na kuchukua hatua za kisheria kwa madereva wote wa wanaolalamikiwa kuendesha mwendo kasi katika barabara ya Mpanda kuelekea majalila.
Mhe.Mwanamvua ametoa maagizo hayo baada ya kupokea changamoto kutoka kwa Baadhi ya Wananchi wakilalamikia baadhi ya madereva wa vyombo vya usafiri hususani gari za abiria pamoja na gari za Serikali kuendesha mwendo kasi bila kujali usalama wa maisha ya Wananchi wanaoishi katika maeneo pembezoni mwa barabara hiyo.
Mnesor Iddi Kombakusha Mkazi wa Majalila Wilayani Tanganyika amesema kuwa baadhi ya madereva wanaotumia Njia hiyo wamekuwa wakihatarisha maisha ya wakazi wa eneo hilo kwa kuendesha Mwendok kasi jambo ambalo linaleta hofu kwa usalama wa waenda kwa miguu wanaotumia barabara hiyo.
Kombakusha amemtaja mmoja wa madereva wanaohatarisha usalama wa Wananchi wa Majalila anayefahamika kwa jina moja la Iddi ambaye amekuwa akiendesha mwendo kasi katika barabara hiyo.
Bw.Kombakusha pia amesema madereva wa magari ya Serikali wanaotumia njia hiyo pia wamekuwa wakikiuka sheria za usalama wa barabarani ambapo wamekuwa wakiendesha mwendo kasi katika maeneo hayo bila kujali kuwa ni maeneo ya makazi.
Mpanda-Katavi (Mkoani Area)
Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi
simu: 025-2957108
Mobile:
Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz
Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved