• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

RC Katavi akabidhi pikipiki 8 kwa Maafisa Tarafa. Awataka kutumia vyombo hivyo kufuatilia Ugawaji wa Mbolea,Uripoti wa Wanafunzi Mashuleni.

Posted on: January 13th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko akikabidhi pikipiki kwa mmoja wa Maafisa Tarafa Mkoani Katavi Leah Gawaza,Afisa Tarafa kutoka Tarafa ya Misunkumilo wakati wa hafla  ya kukabidhi pikipiki 8 kwa Maafisa Tarafa Mkoani Katavi 13 Januari 2022.


Na:OMM- Katavi.

Mkuu wa  Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua  Hoza Mrindoko leo 13 Januari 2023 amekabidhi Pikipiki 8 kwa Maafisa Tarafa wa Mkoa wa Katavi zenye Thamani ya Zaidi ya Shilingi  Milioni 40 kama vitendea kazi ili kurahisisha Utekelezaji wamajukumu mbalimbali kwa Maafisa hao.

Akizungumza wakati wa kugawa pikipiki hizo Mkuu wa Mkoa Mrindoko amewataka Maafisa Tarafa waliokabidhiwa pikipiki hizo kutumia vyombo hivyo vya usafiri kwa shughuli zilizokusudiwa ili kurahisisha utekelezaji wa shughuli mbalimbali zikiwemo maagizo mbalimbali ya Serikali.

Amewataka Maafisa Tarafa kutumia vyombo hivyo vya Usafiri kufanya ufuatiliaji wa karibu wa Mwenendo wa Wanafunzi kuripoti Mashuleni katika kipindi hiki cha kuanza muhula wa Masomo 2023 kwa kidato cha kwanza pamoja na kufuatilia kwa karibu mwenendo wa uandikishaji Wanafunzi wa Darasa la kwanza katika mhula wa mMsoko 2023.

Aidha amewasisitiza Maafisa Tarafa hao kufanya ufuatiliaji wa karibu kuhakikisha kuwa mbole ya ruzuku inagawiwa kwa Wananchi pamoja na kuhakikisha kuwa Maafisa Ugani wanatimiza wajibu wao katika utoaji elimu kwa Wananchi kuhusu kilimo cha kisasa.

Awali Katibu tawala Mkoa wa Katavi Bw.Hassan Abas Rugwa ameeleza lengo la Serikali Mkoani Katavi   kutoa pikipiki hizo kwa Maafisa Tarafa ni kuhakikisha Maafisa hao wanatekeleza majukumu yao kikamilifu hasa katika kipindi hiki cha msimu wa Kilimo ambapo Maafisa hao wana wajibu mkubwa wa kuhakikisha kuwa mbolea ya Ruzuku inawafikia Wananchi ipasavyo pamoja na kusimamia ufuatiliaji wa Wanafunzi kuripoti shuleni kwa ajili ya kuanza Masomo.

“Hiki tunachokifanya leo ni Matokeo ya mpango wa Mkoa ambapo katika Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2022/2023 Mkoa ulitenga Jumla ya Shilingi Milioni Arobaini na Nne na Laki nne na Elfu Arobaini kwa ajili ya Ununuzi wa Pikipiki.Mkoa wa Katavi unazo Tarafa 10 sasa kutokana na mabadiliko ya Bei tumepata Pikipiki 8 kwa ajili ya Kata Nane ambazo ni Kashaulili,NsimboMisunkumilo,Kabungu,Mwese,Inyonga,Karema,Mamba, na Inyonga ambapo kwa Tarafa za Mpimbwe na Ndurumo zitanunuliwa katika mwaka ujao wa Fedha”Alisema Katibu Tawala Rugwa.

Baadhi ya Maafisa Tarafa waliokabidhiwa pikipiki hizo wameishukuru Serikali  kwa kujenga mazingira wezeshi  ya kuweza  kutekeleza majukumu yao ipasavyo ambapo wameahidi kufanya kazi kwa bidii na kuwatumikia Wananchi wa Mkoa wa Katavi kwa nguvu zote.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved