• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

Posted on: April 3rd, 2025

Aprili 03, 2025.


Wataalamu wa Sekretarieti ya Mkoa na Halmashauri za Mkoa wa Katavi wamepatiwa mafunzo kuhusu uibuaji na utekelezaji wa miradi kwa mfumo wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko, amesema kuwa Mkoa wa Katavi una fursa nyingi za uwekezaji zinazoweza kutekelezwa kwa mfumo wa PPP. Amesisitiza kuwa kupitia mfumo huo, sekta binafsi inaweza kushirikiana na serikali kuwekeza katika miradi mbalimbali ya maendeleo kwa manufaa ya wananchi.

Aidha, amebainisha kuwa Mkoa wa Katavi uko tayari kusimamia uibuaji na utekelezaji wa miradi ya PPP kwa kuhakikisha kuwa wananchi wenye sifa wanahamasishwa kushiriki kikamilifu. Amesisitiza dhamira ya mkoa katika kusaidia juhudi za Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kufanikisha maendeleo ya kiuchumi kupitia miradi ya PPP.

Kwa upande wake, Dkt. Bravious Kahyoza ameeleza kuwa mfumo wa PPP ni nyenzo muhimu ya kuharakisha maendeleo kwa kushirikisha sekta binafsi katika utekelezaji wa miradi ya umma. Amefafanua kuwa sekta binafsi inaweza kushiriki kwa njia mbalimbali, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa miundombinu mipya na kuiendesha kwa niaba ya serikali, utoaji wa huduma kwa kutumia miundombinu iliyopo, na ukarabati pamoja na uendeshaji wa miundombinu ya serikali kupitia makubaliano maalum.

Akizungumzia faida za PPP, Dkt. Kahyoza ametaja kuwa mfumo huu huongeza ujuzi na ubunifu, hususan katika matumizi ya teknolojia, huimarisha ufanisi wa utoaji wa huduma, huongeza rasilimali fedha, na huchangia katika utunzaji bora wa mali za serikali.

Mafunzo haya yameleta mwanga kwa wataalamu wa Sekretarieti ya Mkoa na halmashauri za Mkoa wa Katavi juu ya fursa zilizopo kupitia mfumo wa PPP. Matarajio ni kuwa mafunzo haya yatawawezesha wataalamu hao kushiriki kikamilifu katika uibuaji wa miradi bora ya maendeleo kwa manufaa ya wananchi wa Mkoa wa Katavi.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved