• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

NANENANE MBEYA: SERIKALI KUBORESHA UPATIKANAJI WA ARDHI KWA VIJANA KUPITIA BENKI MAALUM YA ARDHI.

Posted on: August 2nd, 2025

Serikali imetoa maelekezo kwa wakuu wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kuhakikisha kuwa ardhi haizuii wawekezaji vijana, pamoja na kuanzisha Benki ya Ardhi itakayowezesha vijana kukodishiwa ardhi kwa mikataba maalum kwa ajili ya uwekezaji wa kilimo.

Maelekezo hayo yametolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, kupitia taarifa iliyosomwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa, wakati wa ufunguzi wa maonesho ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya John Mwakangale, Jijini Mbeya, tarehe 2 Agosti 2025.

Taarifa hiyo imetoa maagizo kwa Wakuu wa Mikoa ya Katavi, Rukwa, Songwe, Ruvuma, Mbeya, Iringa, na Njombe, ikiwa ni pamoja na kuweka mkazo kwenye matumizi bora ya ardhi, matumizi sahihi ya viuatilifu na kemikali, usalama wa chakula katika ngazi ya kaya, kuepuka uvunaji wa mazao kabla ya wakati, na matumizi ya ardhi kwa ajili ya vijana wawekezaji.

Serikali imesisitiza kuwa kutokana na ongezeko la wawekezaji vijana, kuna haja ya kutenga ardhi kwa ajili yao ili waweze kushiriki kikamilifu katika shughuli za kilimo. Halmashauri zimetakiwa kutenga angalau hekta 100 kwa ajili ya vijana hao, kwa mikataba maalum, kama njia ya kuongeza mapato ya halmashauri na kuwezesha uwekezaji wa vijana kupitia benki ya ardhi.


Aidha, viongozi wa mikoa wameelekezwa kusimamia matumizi sahihi ya ardhi ili kuepusha migogoro kati ya wakulima na wafugaji pamoja na kuzuia uvamizi wa maeneo ya mapito ya wanyama pori kama tembo, hali ambayo imekuwa ikisababisha madhara kwa binadamu na mazingira.


Viongozi wa dini na kimila wameombwa kushirikiana na serikali katika kutoa elimu kuhusu usalama wa chakula kwa wananchi, kwa kusisitiza umuhimu wa kuhifadhi chakula kwa matumizi ya muda mrefu katika ngazi ya kaya, ili kupunguza athari za baa la njaa.


Viongozi wa mikoa wameelekezwa pia kusimamia kwa karibu uvunaji wa mazao ya biashara kama pareto, ili kuhakikisha kuwa yanavunwa kwa wakati unaofaa, hatua itakayosaidia kuongeza ubora wa mazao hayo na thamani katika soko la ndani na nje ya nchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • BENKI YA CRDB YATOA MSAADA WA MADAWATI SHULE YA WASICHANA KATAVI

    August 12, 2025
  • RC MRINDOKO AZIAGIZA HALMASHAURI ZOTE KATAVI KUSAMBAZA MBEGU BORA ZA UFUTA KWA WAKULIMA ILI KUONGEZA UZALISHAJI MSIMU UJAO.

    August 08, 2025
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA MPANDA YANG’ARA NANENANE 2025, YASHIKA NAFASI YA TATU.

    August 08, 2025
  • MRINDOKO AHIMIZA UBUNIFU NA ABAINISHA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOANI KATAVI.

    August 06, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved