• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

MKUU WA MKOA KATAVI APIGA STOP UNYANYASAJI SEHEMU ZA KAZI

Posted on: May 1st, 2023

RC KATAVI APIGA STOP UNYANYASAJI SEHEMU ZA KAZI

Kazi ni sehemu ya asili ya binadamu wote duniani. Kazi ni maendeleo; humletea heshima na shibe mtu nyumbani kwake, husaidia mwili kuwa na afya njema.

Kazi huondoa fedheha, umaskini na ukoloni mamboleo. Kazi ina manufaa makubwa kwa mwanadamu, binadamu wote duniani hatuna budi kuithamini na kuiheshimu kazi.

Mataifa yote duniani yanaheshimu na kutahamini kazi kwa sababu huleta maendeleo katika mataifa na katika maisha ya mwanadamu.

Nchini Tanzania , tuliazimia kufanya kazi ili kujiletea maendeleo mara baada ya kupata uhuru wetu. Tulihamasishana, uhuru bila kazi hauna maana katika maisha yetu, kama taifa lazima tufanye kazi.

Karibu miongo 6 ya uhuru wetu kama taifa, Tanzania tumepiga hatua kubwa ya kimaendeleo kutokana na kufanya kazi. Tuna vituo vingi vya kutolea afya, tuna dawa na vifaa tiba katika hospitali zetu, tuna mtandao mkubwa wa barabara, madaraja, viwanja vya ndege na bandari, tuna miundombinu ya elimu na vifaa mbali mbali vya kufundishia katika shule zetu. Tuna mambo mengi ya kimaendeleo katika nchi yetu.

Katika Mkoa wa Katavi tunajivunia maendeleo lukuki. Kwa kutaja machache, tuna hospitali na vituo vya kutolea huduma ya afya kwa wananchi wetu, tuna bandari, tuna kiwanja cha ndege, tuna barabara na bandari, tuna chakula cha kutosha kwa wananchi wetu.

Bidii na maarifa ya kazi kwa wafanyakazi wa umma, sekta binafsi kwa kushirikiana na wananchi wa Mkoa wa Katavi umepata maendeleo makubwa katika sekta mbali mbali.

Katika maadhimisho ya kumbukizi ya Siku ya wafanyakazi duniani, yaliyoadhimishwa kimkoa katika Viwanja vya Shule ya Msingi Kashaulili, Mjini Mpanda, Kiongozi Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe. Mwanamvua Mrindoko, kwa dhati ya moyo wake, hakusta kuwapongeza wafanyakazi wote katika mkoa wake kwa kazi nzuri waliyofanya katika kuwahudumia wananchi wa mkoa huo.

Mhe. Mrindoko amewataarifu wafanyakazi kuwa kazi wanazozifanya katika mkoa wake ndizo ambazo zimeleta mafanikio makubwa na kuuheshimisha mkoa.  

Amebainisha kazi hizo kuwa ni pamoja na utekelezaji wa Ilani ya CCM, utoaji wa huduma na utatuzi wa kero mbali mbali kwa wananchi.

Kiongozi huyo, amewasihi wanafanyakazi kuendelea kufanya kazi kwa bidii na maarifa, nidhamu ya hali ya juu, kujituma na kutumia muda wao vizuri katika utoaji wa huduma kwa wananchi wa mkoa wake.

Amewaahidi wafanyakazi hao kuwa serikali ya mkoa wake itaendelea kuweka mazingira mazuri ya kazi kwa wafanyakazi wote ili kuwezesha mipango, programu na miradi ya maendeleo kusonga mbele zaidi.

Amewaonya waajiri wote katika mkoa wake kutojihusisha na unyanyasaji wa wafanyakzi wao, kudumisha staha sehemu za kazi, nidhamu na kuwathamini na kuwaheshimu wafanyakazi wote kwa mujibu wa Sheria, Kanununi, Taratibu, Miongozo, Mila na Desturi za kitanzania.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved