• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

MAADHIMISHO SIKU YA MTOTO AFRIKA, CHAGULAGA BADO NI KILIO KWA WASICHANA KATAVI.

Posted on: June 16th, 2025

Katika kuadhimisha siku ya mtoto wa Afrika mkoani Katavi, Mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph kwaniaba ya mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amewaelekeza wakuu wa shule, maafisa elimu pamoja na wakuu wa idara za elimu katika mkoa huo kuhakikisha wanaweka sheria za shule ambazo zinatekelezeka ili kulinda usalama wa watoto wawapo shuleni.

Maagizo hayo ameyatoa leo Juni 16,2025 wakati wa sherehe za maadhimisho ya Mtoto wa Afrika kimkoa yaliyofanyika katika halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika ambapo amesema Serikali inalenga kumlinda mtoto dhidi ya ukatili. 

"Kusimamia maadili na nidhamu itasaidia watoto kuzingatia masomo na kuwaepusha kutumia muda mwingi kufanya matendo vya uovu na pia wazazi endeleeni kuhakikisha ulinzi wa watoto ikiwemo kuwasimamia katika matumizi ya simu, muwaepushe na mitandao ya kijamii," Amesema Mhe. Jamila.

Akisoma Risala ya baraza la watoto Mkoa wa Katavi Maria Samike amesema zipo changamoto mbalimbali katika jamii ambazo zimefanya watoto washindwe kupata haki za msingi pamoja na kuzifikia ndoto zao.

Miongoni mwa changamoto hizo ameziainisha kuwa ni uelewa mdogo wa jamii juu ya umuhimu wa elimu, umaskini, migogoro ya ndoa inayosababisha wazazi kutengana, mimba za utotoni na ukatili wa kijinsia hasa (vipigo, ubakaji, ulawiti).


"Bado jamii zetu zinaendeleza mila zenye kuleta Madhara, imani za kishirikina na mila potofu ikiwemo chagulaga kwa wasichana ambayo imekuwa ikikatisha ndoto za wasichana wengi," Amesema Maria.

Kwa upande mkuu wa wilaya ya Tanganyika Onesmo Busweru amesema serikali imewekeza katika kuwajenga walimu na walezi katika kuhakikisha watoto wanakuwa salama. Na amewataka watoto kuitunza na kuitetea serikali na kuwa wazalendo wasichochewe katika kuleta vurugu watakapokuwa wakubwa.


Maadhimisho siku ya mtoto wa Afrika 2025 yanabebwa na kauli mbiu isemayo Mtoto:Tulipotoka, Tulipo na Tuendako.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO SIKU YA MTOTO AFRIKA, CHAGULAGA BADO NI KILIO KWA WASICHANA KATAVI.

    June 16, 2025
  • RC MRINDOKO ATOA WITO KWA VIONGOZI KUHAMASISHA MATUMIZI YA CHAKULA CHENYE VIRUTUBISHI ILI KUTOKOMEZA UDUMAVU.

    June 10, 2025
  • RC MRINDOKO AZINDUA MSIMU WA UNUNUZI WA PAMBA NA MAZAO MENGINE KWA MWAKA 2025/26

    June 09, 2025
  • RC MRINDOKO AKUTANA NA WAENDESHA BODABODA KATAVI, ATOA WITO WA AMANI NA USHIRIKI UCHAGUZI MKUU 2025.

    June 05, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved