• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

KIKAO CHA TATHMINI YA LISHE CHAFANYIKA KATAVI RC KATAVI AHIMIZA ELIMU YA LISHE KWA WANANCHI, ASISITIZA UTEKELEZAJI WA BAJETI AFUA ZA LISHE KWA HALMASHAURI

Posted on: January 31st, 2023

Na:OMM- Katavi

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Hoza Mrindoko ametoa siku 7 kwa Halmashauri zote  Mkoani humo kuhakikisha Fedha zote zilizotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa Afua za Lishe  zinatumika kama ilivyokusudiwa.

Mhe.Mrindoko ametoa agizo hilo Februari 1, 2022 katika kikao cha Tathmini ya Lishe kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda kilichokutanisha Wadau mbalimbali wa  lishe  Mkoani humo.

“Tumegundua kuwa Halmashauri zetu zote bado hazijaweza kutoa kwa kiasi kile kilichopangwa Fedha za mapato ya ndani ambazo zimekusudiwa na zimeelekezwa kwenda kufanya kazi katika  Afua za Lishe na hilo linatokana na uzembe wa kusimamia vizuri, hivyo tumeelekeza ndani ya siku 7 Halmashauri zote zikahakikishe Fedha zote zilizotengwa kwa ajili ya afua za Lishe zinatumika kama ilivyokusudiwa.”Alisema Mkuu wa Mkoa Mrindoko.

Aidha Mkuu wa Mkoa Mrindoko amewaagiza Wakurugenzi na Waganga wakuu wa Halmashauri Mkoani humo kutoa maelezo kwa  Maandishi kwa nini wasichukuliwe  hatua za kinidhamu kwa kushindwa kusimamia kikamilifu utekelezaji wa Bajeti ya Afua za Lishe  kwa kipindi cha miezi 6  kuanzia Julai 2022 hadi Disemba 2022.

Katika hatua nyingine Mhe.Mrindoko amewaelekeza Wataalamu wa Afya akuandaa vipeperushi vitakavyoainisha  makundi mbalimbali ya chakula kulingana na mazao yanayolimwa ndani ya Mkoa wa Katavi na kusambaza kipeperushi hicho kwa Wananchi ili kujenga uelewa wa namna ya Ulaji kwa kuzingatia Lishe Bora kusudi kuondokana na changamoto ya udumavu na ukondefu.

Kwa Upande wake Afisa Lishe Mkoa wa Katavi Bi.Asnati Mrema amesema wataalamu wa Mkoa   wamepokea wamejipanga kutekeleza kikamilifu maagizo yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa.

“Tulikuwa tunafanya tathmini ya mkataba wa Lishe kwa Miezi 6 ambapo tumepitia tumepitia mkataba na kuona utekelezaji wa viashiria vyote ndani ya Mkataba lakini katika kiashiria cha Fedha ndio kiashiria ambacho kama Mkoa hatukufanya vizuri ambapo Mkuu wa Mkoa ameagiza kiashiria cha Fedha kifanyiwe maboresho”Alisema Bi.Asnath Mrema.

Ameeleza kuwa Mkoa wa Katavi unazalisha kwa wingi  lakini una changamoto ya udumavu kwa Asilimia 33, Tumejipanga kuhakikisha kuwa Elimu ya Lishe kwa Wananchi inatolewa kikamilifu kwa Wananchi kuzingatia muongozo ulitolewa na Wizara ya Afya ambapo mikutano ya hadhara,vyombo vya habari na njia nyinginezo zitatumika katika kuhakikisha Elimu ya Lishe inawafikia Wananchi.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved