• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

KATAVI YAANZA KUYABAINISHA MAENEO HATARISHI YANAYOCHOCHEA MAGONJWA YA MLIPUKO.

Posted on: July 22nd, 2025

Sekta ya afya Mkoa wa Katavi imeanza hatua za awali za kutekeleza mkakati wa kukabiliana na magonjwa mapya ya mlipuko na yanayojirudia rudia kwa kuyatambua maeneo hatarishi yanayochochea kuendelea kuwepo kwa magonjwa hayo.

Utelekezaji wa mikakati hiyo umetangazwa rasmi na Mganga mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt Jonathan Budenu katika kikao cha tathimini ya huduma za usafi wa afya mazingira pamoja na huduma za maji safi na vyoo vijijini kilichofanyika leo Julai 22,2025, ambapo amesema lengo ni kufikia makubaliano ya kile kinachoenda kufanyika katika jamii ili iweze kupata uelewa kuhusu afya mazingira.

“Tukiyatambua maeneo yote ambayo ni hatarishi kwa magonjwa ya mlipuko, itasaidia kuweka mkakati wa pamoja wa kukabiliana na magonjwa hayo lakini pia kila mmoja aliyetoka katika halmashauri akafanye upembuzi ili kubainimaeneo hayo na tuweze kuwa na mkakati wa pamoja ili kuhakikisha tunafikia malengo ya kila mtanzania kuwa anapata huduma bora za afya,” amesema Dkt Budenu.

Akizungumza na waganga wakuu wa Halmashauri pamoja na maafisa afya katibu tawala Mkoa wa Katavi, Albert Msovela amewataka kuendelea kuchukua tahadhari na kujikinga dhidi ya magonjwa ya mlipuko kwa kujenga uelewa mpana wa matumizi ya vyoo bora katika jamii.

“Hali ya uwepo wa vyoo bora bado hairidhishi, kwa mwananchi wa kawaida anaweza kuona ni hali ya kawaida lakini ukiwaza kwanini tunakuwa na mlipuko wa magonjwa ni kwa sababu hatuna matumizi sahihi ya vyoo ambavyo vipo, Madhara yake tumeyaona kutokana hali ya magonjwa ya mlipuko inavyokuwa kwenye jamii,” amesema Msovela.

Akizungumza kwaniaba ya washiri wa kikao hicho Dkt. Alex Mrema, ameahidi kwenda kuyafanyia kazi yale yote yaliyoelekezwa ili kufikia malengo ya serikali ya kuhakikisha wanaweka mikakati thabiti ya kutokomeza magonjwa ya mlipuko.

Takwimu za uwepo wa vyoo bora ngazi ya kaya zinaainisha kuwa mkoa wa Katavi unajumla ya 66.3% ya vyoo bora sawa na idadi ya kaya 129,646 idadi ya kaya zinazotumia vitakasa mikono ni 48.43% na kaya ambazo hazina vyoo ni asilimia 0.1% pekee.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • SEPTEMBA 2025, MWISHO WA MATUMIZI YA MKAA NA KUNI KWENYE TAASISI ZINAZO HUDUMIA WATU ZAIDI YA 100. HUDUMIA

    July 23, 2025
  • KATAVI YAANZA KUYABAINISHA MAENEO HATARISHI YANAYOCHOCHEA MAGONJWA YA MLIPUKO.

    July 22, 2025
  • HUDUMA YA KUCHUJA DAMU (DIALYSIS): TUMAINI JIPYA KWA WAGONJWA WA FIGO KATAVI.

    July 21, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WATAKIWA KUTUMIA MADHABAHU KUKEMEA NA KUELIMISHA UMMA JUU YA MADHARA YA RUSHWA KATIKA UCHAGUZI.

    July 18, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved