• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

HALMASHAURI YA MANISPAA YA MPANDA YANG’ARA NANENANE 2025, YASHIKA NAFASI YA TATU.

Posted on: August 8th, 2025

Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda imeibuka nafasi ya tatu kati ya halmashauri zilizofanya vizuri katika maonesho ya kilimo, mifugo na uvuvi ya Nanenane 2025 Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, yaliyohitimishwa leo katika viwanja vya John Mwakangale, jijini Mbeya.

Tuzo ya ushindi imepokelewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda, Bi. Sophia Kumbuli ambaye amekabidhiwa na Mgeni Rasmi wa hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Mhe. Charles Makongoro Nyerere, mbele ya umati wa washiriki na wageni waalikwa.

Katika matokeo ya mwaka huu, Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa imeibuka kinara kwa nafasi ya kwanza, ikifuatiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Iringa katika nafasi ya pili. Ushindi wa Mpanda unatajwa kuwa umetokana na maandalizi thabiti, mshikamano wa wataalamu wake na ubunifu wa kuonesha teknolojia rafiki na zenye tija kwa sekta ya kilimo na mifugo.


Maonesho ya mwaka huu yamebeba kaulimbiu isemayo: “Chagua viongozi bora kwa maendeleo endelevu ya kilimo, mifugo na uvuvi.” Kaulimbiu hii imetoa ujumbe mahsusi kwa wadau wote wa sekta hizi muhimu, ikiwataka kuweka kipaumbele kwa uongozi wenye dira na maono ya maendeleo.


Kupitia ushindi huu, Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda imeonesha dhamira yake ya kuendelea kuwa mstari wa mbele katika kukuza sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi, na kutoa mchango wa moja kwa moja katika maendeleo ya wananchi wake na taifa kwa ujumla.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • BENKI YA CRDB YATOA MSAADA WA MADAWATI SHULE YA WASICHANA KATAVI

    August 12, 2025
  • RC MRINDOKO AZIAGIZA HALMASHAURI ZOTE KATAVI KUSAMBAZA MBEGU BORA ZA UFUTA KWA WAKULIMA ILI KUONGEZA UZALISHAJI MSIMU UJAO.

    August 08, 2025
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA MPANDA YANG’ARA NANENANE 2025, YASHIKA NAFASI YA TATU.

    August 08, 2025
  • MRINDOKO AHIMIZA UBUNIFU NA ABAINISHA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOANI KATAVI.

    August 06, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved