• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

BENKI YA CRDB YATOA MSAADA WA MADAWATI SHULE YA WASICHANA KATAVI

Posted on: August 12th, 2025

Benki ya CRDB Mkoa wa Katavi imetoa madawati 60 kwa Shule ya Sekondari ya Wasichana Katavi, iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, ikiwa ni sehemu ya mpango wa benki hiyo wa kurudisha fadhila kwa wananchi kupitia faida iliyopatikana.

Akikabidhi madawati hayo, Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Bi Jennifer Tondi, ameeleza kuwa Benki ya CRDB kupitia mkakati wake wa Keti Jifunze itaendelea kushirikiana na serikali katika kuchangia huduma mbalimbali za kijamii mkoani Katavi.

Amesema kuwa pamoja na majukumu yake ya kibenki, benki hiyo imetenga asilimia moja ya faida yake ili kuhudumia mahitaji ya jamii katika sekta mbalimbali, ikiwemo elimu.

Aidha, ameeleza kuwa lengo ni kuhakikisha tatizo la wanafunzi kuketi chini linaondolewa kabisa kupitia kampeni ya Keti Jifunze, na kwamba benki itaendelea kushughulikia changamoto ya upungufu wa madawati mashuleni kadri faida itakavyopatikana.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Mhe. Jamila Yusuph, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi, ameishukuru Benki ya CRDB kwa mchango wake katika maendeleo ya wilaya hiyo, amewataka wadau wengine kuendelea kujitokeza kuchangia maendeleo, na amewasisitiza wanafunzi kusoma kwa bidii pamoja na kuyatunza madawati hayo ili yaweze kusaidia vizazi vijavyo.

Aidha, ametoa wito kwa wanafunzi hao kuepuka mahusiano ya kimapenzi katika kipindi cha masomo yao, akisisitiza kuwa kufanya hivyo kutawawezesha kuzingatia elimu na kujiepusha na changamoto zinazoweza kuhatarisha maisha yao ya baadaye.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • BENKI YA CRDB YATOA MSAADA WA MADAWATI SHULE YA WASICHANA KATAVI

    August 12, 2025
  • RC MRINDOKO AZIAGIZA HALMASHAURI ZOTE KATAVI KUSAMBAZA MBEGU BORA ZA UFUTA KWA WAKULIMA ILI KUONGEZA UZALISHAJI MSIMU UJAO.

    August 08, 2025
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA MPANDA YANG’ARA NANENANE 2025, YASHIKA NAFASI YA TATU.

    August 08, 2025
  • MRINDOKO AHIMIZA UBUNIFU NA ABAINISHA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOANI KATAVI.

    August 06, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved