• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

722 Wafanyiwa Ukatili Katavi. Jamii Katavi yahimizwa kukemea,kukomesha Vitendo vya Ukatili.

Posted on: November 25th, 2022

722 Wafanyiwa Ukatili Katavi.

Jamii Katavi yahimizwa  kukemea,kukomesha  Vitendo vya Ukatili.

 Jumla ya watu 722 wameripotiwa kufanyiwa vitendo vya  ukatili wa kijinsia ambapo  ndani ya saa 72 kesi 63 za ukatili wa kijinsia ziliripotiwa kwa kipindi cha Mwaka 2021 Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Katavi Bi Anna Shumbi ameeleza.

Akitoa hotuba  kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe Mwanamvua Mrindoko mbele ya wakazi wa Mtaa wa Rungwa katika uzinduzi wa kampeni ya Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia 25 Novemba 2022,  Afisa maendeleo ya Jamii mkoa ameeleza kuwa matukio ya ukatili wa Kijinsia  yaliyoongoza zaidi ni ukatili wa kisaikolojia  na lugha ya matusi ambao ulikuwa ni kesi 396,ukatili wa kimwili hasa kipigo kesi 248 na ukatili wa kingono kesi 78 kwa mwaka 2021.

Ameeleza kuwa chanzo cha ukatili wa kijinsia hususani kwa watoto ni Familia huku maeneo mengine ambako ukatili hufanyika kwa kiasi kikubwa kuwa ni Migodini Masokoni na kwingineko hivyo ni muhimu Jamii kuchukua hatua za makusudi kupunguza na kuondoa kabisa matukio ya vitendo vya ukatili unaofanywa kwa Watoto na Wanawake.

Ametadharisha Wananchi kuchukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kufanya usafi wa mazingira haswa katika kipindi cha masika ili kuondoa mazingira ya vichaka yanayoweza kushawishi wasio na nia njema kufanya vitendo vya Ukatili kwa Wanawake na watoto pamoja na kuepuka kuwatuma watoto nyakati za Jinoni.

Kwa Upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Mpanda Sophia Kumbuli amesema ni muhimu Jamii kuelekeza nguvu katika  mapambano ya  ukatili wa Kijinsia kwa watoto wa kiume pia  badala ya wa kike na wanawake  peke yake kwa kuwa watoto wa kiume nao  wamekuwa wahanga wakubwa wa vitendo vya ukatili ambapo baadhi wamekuwa wakifanyiwa vitendo visivyofaa ikiwemo kulawitiwa na mengine mengi.

Maadhimisho hayo ya kupinga ukatili wa kijinsia  kwa watoto na Wanawake yaliyozinduliwa 25 Novemba 2022  yanayoadhimishwa na Serikali kwa kushirikiana na Asasi mbalimbali zisizo za kiserikali  yatadumu kwa siku 16 ambapo kilele chake kitakua 10 Desemba, 2022 yakibebwa na kaulimbiu inayosema Kila uhai una thamani tokomeza mauaji na ukatili kwa Wanawake  Watoto.








Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved