• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

RC MRINDOKO AAGIZA WAFANYABIASHARA KATAVI KUTOPANDISHA BEI WAKATI WA MFUNGO WA KWARESMA NA RAMADHANI.

Posted on: February 19th, 2026

Wakati waumini wa dini za Kikristo na Kiislamu wakiingia katika kipindi cha mfungo wa Kwaresma na Ramadhani, Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko, amewataka wafanyabiashara kuhakikisha hawapandishi bei za bidhaa, akisisitiza kuwa mkoa wa Katavi una chakula cha kutosha na bidhaa zinapatikana kwa urahisi.

Akizungumza leo, Februari 19, 2025 wakati wa mkutano wake na wafanyabiashara wa Soko Kuu la Manispaa ya Mpanda, RC Mrindoko amesema lengo la kufika sokoni hapo ni kusikiliza kero na changamoto wanazopitia wafanyabiashara pamoja na kufuatilia mwenendo wa bei za bidhaa baada ya kuanza kwa mfungo wa Kwaresma na Ramadhani.

“Nasisitiza wafanyabiashara muendelee na bei zilezile za awali. Mkoa wa Katavi hauna njaa, chakula kipo cha kutosha na hakuna sababu ya kupandisha bei,” amesema RC Mrindoko.


Akiongeza kuwa Serikali haitavumilia upandishaji holela wa bei, huku akiwataka wananchi kutoa taarifa mara moja endapo watakutana na ongezeko la ghafla la bei sokoni.

“Mteja akiona bei imepanda bila sababu, atoe taarifa mara moja kwa mamlaka husika ili hatua zichukuliwe,” amesisitiza.


Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa amemuelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda kuhakikisha kuwa ifikapo Machi 19, 2026, soko hilo linakuwa limefanyiwa ukarabati, akieleza kuwa msimu wa mvua umebainisha changamoto ya mapaa yanayovuja na kuathiri shughuli za biashara.

RC Mrindoko ametumia fursa hiyo kuwatakia waumini wote wa dini za Kikristo na Kiislamu mfungo mwema wa Kwaresma na Ramadhani, akiwataka kuendelea kudumisha amani, mshikamano na upendo katika kipindi chote cha ibada.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • RATIBA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI - MWAKA 2025 April 28, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA SEKTA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI MKOA WA KATAVI August 27, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA SEKTA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI MKOA WA KATAVI August 27, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AWAAGIZA VIONGOZI TANGANYIKA KUTATUA KERO ZA WANANCHI KWA WAKATI

    February 19, 2026
  • RC MRINDOKO AAGIZA WAFANYABIASHARA KATAVI KUTOPANDISHA BEI WAKATI WA MFUNGO WA KWARESMA NA RAMADHANI.

    February 19, 2026
  • UTEKELEZAJI WA BIMA YA AFYA KWA WOTE WAANZA KATAVI

    February 18, 2026
  • WATAALAMU WA ELIMU KUTOKA ZANZIBAR WAVIKA H/W YA MLELE KUJIFUNZA.

    February 05, 2026
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved