• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Katavi Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
  • Services
  • Administration
    • Departments
      • Adm and HR
      • Planning and Coordination
      • LGA.s
      • Infrustructures
      • EPSS
      • Water
      • Healthy
      • Education
    • Units
      • Information and Communication Technology
      • Finance and Accounts
      • Procurement and Management
      • Legal
      • Internal Auditor
    • Organization Structure
  • Publications
    • Guidelines
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events
  • Projects
    • Completed projects
    • On Going Projects
  • Districts
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Tourism
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

UKATILI KWA WATOTO HAUKUBALIKI KWA MWENYEZI MUNGU

Posted on: March 5th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe. Mwanamvua Mrindoko ametoa wito kwa wananchi wote katika mkoa wake kujitokeza kukemea na kulaani vitendo vya ukatili vinavyofanywa na baadhi ya watu dhidi wanafunzi wa shule katika Wilaya ya Mpanda.

Amesema hayo kufuatia uchunguzi wa awali uilofanywa na vyombo vya usalama kuwa kuna ufanyikaji wa mapenzi kinyume na maumbile yaani ulawiti, usagaji na ubakaji katika baadhi ya shule za msingi na sekondari, vituo vya shule ya awali na vya kulelea watoto yatima katika wialya hiyo.

Amefafanua kuwa mapenzi hayo yanawahusisha wanafunzi kwa wanafunzi, baadhi ya walimu na wafanyakazi wanafanya na wanafunzi, baadhi ya watu wazima waliopo mtaani wanafanya mapenzi ya aina hiyo na wanafunzi.

Kwa masikitiko makubwa, Mhe. Mrindoko amesema katika uchunguzi huo ipo orodha ndefu inayoonyesha kuwa kuna ukiukwaji mkubwa wa maadili ndani ya taasisi zake ambazo jamii ina tegemea kuwafundishia watoto wake.

Amesema imebainika kuwa kuna mabweni bubu na shule za msingi binafsi na vituo vya kulelea watoto ambavyo havina vibali na ameagiza kufungwa shule hizo.

Mhe. Mrindoko ameitaka jamii, wazazi/walezi na wananchi wote mkoani kwake kupaza sauti ‘kukataa ulawiti, usagaji na ubakaji katika mkoa wake.

‘Tusipokemea haya watoto wetu wataendelea kuharibiwa na ukatili utaenea katika mkoa wetu’

Tushirikiane kukemea na kuwaelimisha watoto na vijana wetu kwamba mambo hayo siyo utamadauni wetu wala maelekezo ya mwenyezi mungu na hayapo sehemu yoyote duniani na hayana uhalali wowote ule.

Jambo lolote la namna hiyo likitokea sisi wananchi katika ngazi ya familia/ukoo, tusinyamaze, tusikae kimya, tulifikishe kwenye vyombo vya sheria na hatua zichukuliwe dhidi ya watu wote wanaojihusisha na uhalifu huo.

Viongozi wa dini tuwatangazie waumini kuhusu maovu hayo na madhara yake kwa jamii nao pia wayakemee kwa nguvu zote.

Ukaguzi wa shule ufanyike mara kwa mara na hatua zichuliwe dhidi ya shule zinazokiuka maadili na sheria za sekta ya elimu nchini. Tume ya utumishi wa walimu ifanye uchunguzi wa kina kuhusu walimu wanaojihusisha na utovu wa nidhamu mashuleni na kuwachulia hatua za kinidhamu

Jeshi la Polisi katika Mkoa wa Katavi liimarishe madawati ya wanawake na watoto na kuwachukulia hatua za kisheria watu wote wanaojihusisha na vitendo vya ukatili dhidi ya watoto/wananfunzi

Mhe mrindoko ameyasema hayo katika wiki ya maandalizi kuadhimisha siku ya wanawake inayotarajiwa kuadhimishwa katika viwanja vya Mpanda ndogo Wilayani Tanganyika.

Miongoni mwa shughuli zinazoendelea kufanyika kabla ya kilele cha maadhimsho hayo, ni pamoja na kutoa elimu ya lishe, rushwa na kupinga ukatili, kupanda miti, kutembelea vituo vya yatima na kutoa misaada, kuendesha kongamano,maonyesho na mabonanza

Kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2023 ni ‘Mawazo ya ujasiri yenye kuleta teknolojia jumuishi,ubunifu, elimu inayoweza kupambana na ubaguzi na kutengwa kwa wanawake dunaiani kote.  

Announcements

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • View All

Latest News

  • RC MRINDOKO ATOA WITO KWA VIONGOZI KUHAMASISHA MATUMIZI YA CHAKULA CHENYE VIRUTUBISHI ILI KUTOKOMEZA UDUMAVU.

    June 10, 2025
  • RC MRINDOKO AZINDUA MSIMU WA UNUNUZI WA PAMBA NA MAZAO MENGINE KWA MWAKA 2025/26

    June 09, 2025
  • RC MRINDOKO AKUTANA NA WAENDESHA BODABODA KATAVI, ATOA WITO WA AMANI NA USHIRIKI UCHAGUZI MKUU 2025.

    June 05, 2025
  • JAJI MKUU WA TANZANIA ASISITIZA UADILIFU NA USHIRIKIANO WA WADAU KATIKA UTOAJI HAKI.

    May 28, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
More Videos

Quick Links

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Related Links

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Location Map

Contact Us

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Postal Address: Box 235, Mpanda -Katavi

    Telephone: 025-2957108

    Mobile:

    Email: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Katavi RS . All rights reserved.