• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Katavi Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
  • Services
  • Administration
    • Departments
      • Adm and HR
      • Planning and Coordination
      • LGA.s
      • Infrustructures
      • EPSS
      • Water
      • Healthy
      • Education
    • Units
      • Information and Communication Technology
      • Finance and Accounts
      • Procurement and Management
      • Legal
      • Internal Auditor
    • Organization Structure
  • Publications
    • Guidelines
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events
  • Projects
    • Completed projects
    • On Going Projects
  • Districts
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Tourism
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

SERIKALI YANUIA KUWALINDA WAANDISHI WA HABARI KATIKA KIPINDI CHA UCHAGUZI

Posted on: July 10th, 2025


Kuelekea uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, serikali imeweka mikakati Thabiti ya kuhakikisha kuwa katika  kipindi  cha uchaguzi kila mwanahabari anakuwa salama yeye pamoja na vifaa vyake kupitia jeshi la polisi ili waweze kufanya kazi katika mazingira salama, Rafiki na yenye uhuru wakati wakitekeleza majukumu yao.

Mikakati hiyo imetolewa wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Wadau Kujadili Mchango wa Sekta ya Habari katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu 2025, Julai 9, 2025 jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ambapo amewaasa waandishi wa habari nchini kuwa walinzi wa ukweli, wajenzi wa amani na kuchochezi wa uwajibikaji wa kisiasa.

PICHA; Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Dotto Biteko akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Wadau Kujadili Mchango wa Sekta ya Habari katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu 2025.

Ameeleza kuwa Katika kipindi hiki cha uchaguzi wandishi wa habari wanapaswa kuwa walezi wa maudhui ya habari yanayokwenda kwa jamii, mjue kuwa katika habari hizo taifa litabaki moja aidha limegawanyika, hivyo wanawajibu wa kuwa walinzi wa kweli na wajenzi wa amani huku wakiwabaini wachochezi katika tasnia ya habari na kuwawajibisha bila kusubiri vyombo vya dola.

Amevitaka vyombo vya habari kuwa kioo cha jamii na kujiepusha na uzushi, chuki au upendeleo na badala yake kuhimiza maelewano, uvumilivu wa kisiasa, na utamaduni wa kuheshimu tofauti za maoni.

"Ni wajibu wa Serikali kuhakikisha waandishi wa habari katika kipindi chote cha mchakato wa uchaguzi wanabaki salama pamoja na vitendea kazi vyao. Aidha, Serikali, tutaendelea kulisimamia hili kwa nguvu zetu zote. Tutahakikisha kuwa, mnakuwa na mazingira salama, huru na rafiki wakati wote wa majukumu yenu,". amesema Dkt. Biteko

.

PICHA; Baadhi ya wajumbe waliohudhuria wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Wadau Kujadili Mchango wa Sekta ya Habari katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu 2025.

Ameendelea kusema kuwa  kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 katika jamii kutakuwa na watu wenye mitazamo tofauti kulingana na vipaumbele vyao hata hivyo vyombo vya habari vina fursa ya kutoa uelekeo kwa taifa.

"Uchaguzi ni kipindi cha muda mfupi, tumuombe Mungu hata baada ya Uchaguzi tubaki kuwa Taifa moja lenye ustahimilivu na kila mmoja akitoka kwake aende kutafuta mkate arudi nyumbani kwa familia yake kukiwa na amani, sisi kupitia mkutano huu tuungane kuhakikisha Taifa letu linabaki salama. Sekta ya habari ni nyenzo muhimu katika kulinda na kudumisha amani katika kipindi chote cha uchaguzi," amesisitiza Dkt. Biteko.

PICHA; Baadhi ya wajumbe waliohudhuria wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Wadau Kujadili Mchango wa Sekta ya Habari katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu 2025.

Kutokana na mazingira wezeshi kwa sekta ya habari nchini  idadi kubwa ya vyombo vya habari imeongezeka ukilinganisha na miaka iliyopita, ambapo kuna jumla ya magazeti 375, vituo vya redio 247, vyombo vya habari vya mtandaoni 355, blogs 72 na vituo vya televisheni 68.

MWISHO.

Announcements

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • RATIBA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI - MWAKA 2025 April 28, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA SEKTA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI MKOA WA KATAVI August 27, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA SEKTA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI MKOA WA KATAVI August 27, 2025
  • View All

Latest News

  • RC MRINDOKO AKAGUA MIRADI YA MAJI MPANDA, ATOA MAAGIZO YA KUONGEZA KASI YA UTEKELEZAJI.

    September 03, 2025
  • RC MRINDOKO AHIMIZA AMANI NA USHIRIKIANO KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025.

    September 01, 2025
  • MFUMO WA E - MABORESHO KUIMARISHA UTENDAJI KWA WATUMISHI WA UMMA.

    August 26, 2025
  • MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA YAFIKIA TAMATI, DC BUSWELU AWASISITIZA UZALENDO

    August 26, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
More Videos

Quick Links

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Related Links

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Location Map

Contact Us

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Postal Address: Box 235, Mpanda -Katavi

    Telephone: 025-2957108

    Mobile:

    Email: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Katavi RS . All rights reserved.