• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Katavi Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
  • Services
  • Administration
    • Departments
      • Adm and HR
      • Planning and Coordination
      • LGA.s
      • Infrustructures
      • EPSS
      • Water
      • Healthy
      • Education
    • Units
      • Information and Communication Technology
      • Finance and Accounts
      • Procurement and Management
      • Legal
      • Internal Auditor
    • Organization Structure
  • Publications
    • Guidelines
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events
  • Projects
    • Completed projects
    • On Going Projects
  • Districts
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Tourism
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

RC MRINDOKO AKUTANA NA WAENDESHA BODABODA KATAVI, ATOA WITO WA AMANI NA USHIRIKI UCHAGUZI MKUU 2025.

Posted on: June 5th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko, ameutaka Umoja wa Waendesha Bodaboda mkoani humo kuhakikisha hauhusiki na vitendo vya uvunjifu wa amani, bali uwe sehemu ya kulinda utulivu kwa kutoa taarifa kwa vyombo husika pindi wanapobaini dalili za machafuko katika maeneo yao ya kazi.

Akiwa mgeni rasmi katika mkutano mkuu wa umoja huo uliofanyika leo, Juni 5, 2025, mkoani Katavi, Mkuu wa Mkoa amesema kuwa Serikali itaendelea kushirikiana kwa karibu na kundi hilo la vijana kwa lengo la kuwawezesha kutekeleza majukumu yao katika mazingira salama na yenye heshima. Aidha, ametoa wito kwa viongozi wa umoja huo kuhakikisha wanawaongoza wanachama wao kwa haki, bila upendeleo wala ubaguzi.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa amewahamasisha waendesha bodaboda kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, sambamba na kuhamasisha vijana wenzao kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mchakato huo muhimu kwa mustakabali wa taifa. Amesisitiza kuwa ushiriki wa vijana katika uchaguzi ni wajibu wa kizalendo na mchango mkubwa kwa maendeleo ya demokrasia.

Naye Mwenyekiti wa Umoja wa Waendesha Bodaboda Mkoa wa Katavi, Bw. Isack Daniel Joseph, amepongeza ushirikiano unaoonyeshwa na Serikali na kuahidi kuwa umoja huo utaendelea kuwa mlinzi wa amani mkoani Katavi. Aidha, amesema kuwa vijana wa bodaboda wamejipanga kuhamasisha wenzao kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, kama sehemu ya kuwajibika kwa jamii na taifa.

Kwa upande wake, Katibu wa umoja huo, Bw. Daniel Vagas Sanga, akisoma risala mbele ya mgeni rasmi, amesema kuwa viongozi wamefanikiwa kufungua ofisi ya umoja wa waendesha bodaboda itakayorahisisha utendaji wa shughuli mbalimbali. Aidha, amesema kuwa wamefanikiwa kuandaa rasimu ya katiba ya umoja, ambayo kwa sasa inatumika kama mwongozo mkuu wa uendeshaji wa shughuli za kila siku.

Katika risala hiyo, Serikali pia imeshukuriwa kwa kuwezesha utoaji wa mikopo ya pikipiki 70 kupitia asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri, inayotolewa kwa makundi maalum, hatua iliyosaidia kuimarisha ajira kwa vijana na kuchochea uwajibikaji



Announcements

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • View All

Latest News

  • RC MRINDOKO AKUTANA NA WAENDESHA BODABODA KATAVI, ATOA WITO WA AMANI NA USHIRIKI UCHAGUZI MKUU 2025.

    June 05, 2025
  • JAJI MKUU WA TANZANIA ASISITIZA UADILIFU NA USHIRIKIANO WA WADAU KATIKA UTOAJI HAKI.

    May 28, 2025
  • RC MRINDOKO AKEMEA WAKURUGENZI KUZALISHA MADENI MAPYA KWA WAZABUNI.

    May 22, 2025
  • KATAVI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI.

    May 21, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
More Videos

Quick Links

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Related Links

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Location Map

Contact Us

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Postal Address: Box 235, Mpanda -Katavi

    Telephone: 025-2957108

    Mobile:

    Email: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Katavi RS . All rights reserved.