• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Katavi Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
  • Services
  • Administration
    • Departments
      • Adm and HR
      • Planning and Coordination
      • LGA.s
      • Infrustructures
      • EPSS
      • Water
      • Healthy
      • Education
    • Units
      • Information and Communication Technology
      • Finance and Accounts
      • Procurement and Management
      • Legal
      • Internal Auditor
    • Organization Structure
  • Publications
    • Guidelines
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events
  • Projects
    • Completed projects
    • On Going Projects
  • Districts
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Tourism
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

RC KATAVI AWATAKA WANANCHI KUDUMISHA AMANI

Posted on: April 7th, 2023

 

RC KATAVI AWATAKA WANANCHI KUDUMISHA AMANI


Amani ndiyo msingi mkubwa wa maendeleo duniani. Binadamu au taifa lolote duniani haliwezi kuwa na maendeleo yoyote yale bila kuwa na amani.

Amani huvutia wawekezaji, hujenga mazingira ya uzalishaji, huwawezesha watu kufanya shughuli mbali za kijamii na kiroho mfano kuabudu. Kumbe amani ni muhimu siyo tu katika kuwezesha maendeleo katika jamii bali katika kudumisha maendeleo endelevu.

Hakuna serikali duniani isiyopenda amani na utulivu kwa wananchi wake na mipaka yake. Daima serikali huwahimiza wananchi wake kuimarisha na kudumisha amani kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wenyewe na taifa kwa ujumla.

Serikali duniani zimeweka sheria, kanuni na taratibu ili kuhakikisha kuwa amani na utulivu vinadumishwa kwa wananchi na mipaka yake.

Tanzania ni miongoni mwa serikali duniani zilizojiwekea sheria, kanuni na taratibu kwa ajili ya kuhakikisha kuwa amani na utulivu vinadumu nchini na kwa wananchi wake.

Mkoani Katavi, kiongozi mkuu wa mkoa huo, Mhe. Mwanamvua Mrindoko anajitokeza mbele ya vyombo vya habari kuwapongeza wakristo wote mkoani kwake na taifa kwa ujumla kwa kuendesha mfungo wa kwaresma na kuingia katika sikukuu za pasaka kwa amani na utulivu mkubwa.

Mhe. Mrindoko anasema mkoa umeendelea kuwa salama, tulivu na shwari kutokana na ushirikiano mkubwa ambao wananchi wake wameutoa kwa vyombo vya dola katika kudumisha amani na utulivu.

Katika maadhimisho ya sikukuu za pasaka, kiongozi huyo anatoa maelekezo na tahadhari mbali mbali katika kipindi chote cha maadhimisho ya sikukuu na baada ya sikukuu hizo.

Mhe. Mrindoko anawaonya wananchi wote waliojipanga kufanya fujo na ghasia kwa wakristo wote watakao kuwa kwenye ibada kuwa wasithubutu kufanya hivyo kwa kuwa watajutia kupanga hivyo.

Amesema vyombo vya dola vimejipanga kuhakikisha kuwa usalama na utulivu vinaendelea kuwepo sehemu zote za ibada, majumbani na katika kumbi zote za starehe.

Mhe. Mrindoko amesema vyombo vya dola vitafanya doria na misako sehemu mbali mbali ili kuhakikisha kuwa amani inatamalaki katika mkoa wakati wote wa sikukuu na baada ya sikukuu

Kuhusu watoto na wanafunzi, Mhe Mrindoko amepiga marufuku kwa watoto au wanafunzi kwenda kwenye kumbi za starehe na badala yake wapelekwe kwenye maeneo ya wazi ambapo hakuna uwezekano wa kutokea ajali yoyote

Ameonya wazazi watakaokiuka agizo hilo, vyombo vya dola vitawachukulia hatua za kisheria ili kukomesha tabia hiyo

Pamoja na marufuku hiyo, kiongozi huyo amewatahadharisha wanaoendesha vyombo vya moto kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zote za usalama barabrani ili kuepusha ajali zisizo za lazima katika kipindi na baada ya sikukuu.

Announcements

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • View All

Latest News

  • RC MRINDOKO ATOA WITO KWA VIONGOZI KUHAMASISHA MATUMIZI YA CHAKULA CHENYE VIRUTUBISHI ILI KUTOKOMEZA UDUMAVU.

    June 10, 2025
  • RC MRINDOKO AZINDUA MSIMU WA UNUNUZI WA PAMBA NA MAZAO MENGINE KWA MWAKA 2025/26

    June 09, 2025
  • RC MRINDOKO AKUTANA NA WAENDESHA BODABODA KATAVI, ATOA WITO WA AMANI NA USHIRIKI UCHAGUZI MKUU 2025.

    June 05, 2025
  • JAJI MKUU WA TANZANIA ASISITIZA UADILIFU NA USHIRIKIANO WA WADAU KATIKA UTOAJI HAKI.

    May 28, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
More Videos

Quick Links

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Related Links

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Location Map

Contact Us

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Postal Address: Box 235, Mpanda -Katavi

    Telephone: 025-2957108

    Mobile:

    Email: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Katavi RS . All rights reserved.