• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Katavi Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
  • Services
  • Administration
    • Departments
      • Adm and HR
      • Planning and Coordination
      • LGA.s
      • Infrustructures
      • EPSS
      • Water
      • Healthy
      • Education
    • Units
      • Information and Communication Technology
      • Finance and Accounts
      • Procurement and Management
      • Legal
      • Internal Auditor
    • Organization Structure
  • Publications
    • Guidelines
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events
  • Projects
    • Completed projects
    • On Going Projects
  • Districts
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Tourism
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

MRADI WA BEVAC WABORESHA SEKTA YA UFUGAJI NYUKI MKOANI KATAVI.

Posted on: July 9th, 2025

Mratibu wa Mradi wa BEVAC, Bi. Flosia Vugo, kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi, wamefanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika kutembelea Chama cha Ushirika cha Mazao ya Nyuki na kukagua maendeleo ya ujenzi wa kituo cha usindikaji wa mazao ya nyuki. Kituo hicho kinatarajiwa kuwa nguzo muhimu ya kuongeza thamani ya mazao kama asali na nta, na kuchangia katika kuimarisha uchumi wa wakazi wa eneo hilo. Katika ziara hiyo, jumla ya ndoo 270 zilikabidhiwa kwa chama hicho ili kusaidia shughuli za uvunaji wa asali kwa kutumia njia bora na za kisasa.


Timu hiyo pia ilitembelea eneo la “Manzuki Darasa” ambalo limeandaliwa kwa ajili ya kutoa mafunzo ya nadharia na vitendo kwa wafugaji wa nyuki. Kupitia darasa hilo, wanakikundi hujifunza mbinu bora za ufugaji wa nyuki, utunzaji wa mizinga, na usindikaji wa mazao ya nyuki kwa kuzingatia viwango vya ubora.

Katika hatua nyingine, timu hiyo ilitembelea Kikundi cha Wasakatonge kilichopo Kata ya Sibwesa, ambacho kina jumla ya wanachama 17. Kikundi hicho kilikabidhiwa mizinga 57 ya kisasa, ikiwa ni juhudi za kuongeza uzalishaji wa asali na kuimarisha kipato cha wanakikundi. Hata hivyo, kikundi hicho kilibainisha changamoto kadhaa zinazoathiri utekelezaji wa shughuli zao, ikiwemo upungufu wa mavazi ya kinga kwa ajili ya kuvuna asali na ukosefu wa mashine ya kisasa ya kukamulia asali.

Afisa Mifugo wa Mkoa wa Katavi, Bw. Zidihery Mhando, aliwahimiza wanakikundi kutumia vyema fursa zinazotolewa na mradi huo kwa lengo la kukuza uzalishaji na kuongeza thamani ya mazao ya nyuki. Alisisitiza kuwa sekta ya ufugaji wa nyuki ni mojawapo ya maeneo yenye fursa kubwa ya kiuchumi, hasa kwa vijana na wanawake, na kwamba ushiriki wao kikamilifu katika miradi kama hii utaleta mabadiliko ya kweli ya kiuchumi na kijamii.

Mradi wa BEVAC unaendelea kuwa chachu ya maendeleo kwa wafugaji wa nyuki kwa kuwajengea uwezo wa kuzalisha kwa wingi, kuchakata kwa ubora, na kuuza mazao yao kwa faida, hivyo kuchangia kikamilifu katika kukuza uchumi wa kaya na taifa kwa ujumla.





Announcements

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • View All

Latest News

  • BEVAC YAWEKA MSUKUMO MPYA KWENYE SEKTA YA UFUGAJI NYUKI NSIMBO.

    July 10, 2025
  • SERIKALI YANUIA KUWALINDA WAANDISHI WA HABARI KATIKA KIPINDI CHA UCHAGUZI

    July 10, 2025
  • NDANI YA MIAKA MINNE KATAVI YAPOKEA TRILIONI 1.345

    July 05, 2025
  • MRADI WA BEVAC WABORESHA SEKTA YA UFUGAJI NYUKI MKOANI KATAVI.

    July 09, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
More Videos

Quick Links

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Related Links

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Location Map

Contact Us

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Postal Address: Box 235, Mpanda -Katavi

    Telephone: 025-2957108

    Mobile:

    Email: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Katavi RS . All rights reserved.