• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Katavi Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
  • Services
  • Administration
    • Departments
      • Adm and HR
      • Planning and Coordination
      • LGA.s
      • Infrustructures
      • EPSS
      • Water
      • Healthy
      • Education
    • Units
      • Information and Communication Technology
      • Finance and Accounts
      • Procurement and Management
      • Legal
      • Internal Auditor
    • Organization Structure
  • Publications
    • Guidelines
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events
  • Projects
    • Completed projects
    • On Going Projects
  • Districts
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Tourism
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

KATAVI KUANZA KUTUMIA UMEME WA GRID YA TAIFA MEI 20,2025.

Posted on: May 15th, 2025

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko ametembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme na ujenzi wa vituo vya kupokea, kupoza na kusambaza umeme Inyonga chenye uwezo wa 15MVA  katika eneo la Utende wilayani Mlele mkoani hapa.

Akiwa katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo na miradi ya kimikakati leo Mei 14, 2025 wilayani Mlele Mhe. Mrindoko amesema Mradi huo unatarajiwa kuanza kutumika ifikapo Mei 20, 2025 ambapo pamoja na kuondoa changamoto ya kukatika kwa umeme  utaongeza ari ya uwekezaji kutokana na kuwa gharama za uendeshaji wa miundombinu ya uzalishaji inayotegemea umeme itapungua.

Picha: Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko akizungumza baada ya kukagua Mradi wa Ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme na ujenzi wa vituo vya kupokea, kupoza na kusambaza umeme Inyonga chenye uwezo wa 15MVA  katika eneo la Utende wilayani Mlele.

Mkoa wa Katavi  unatekeleza mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme msonyo wa kilovoti 132 kutoka Tabora hadi Katavi na ujenzi wa vituo vya kupokea, kupoza na kusambaza umeme katika vituo vya Ipole chenye uwezo wa 15MVA, Inyonga chenye uwezo wa 15MVA na Mpanda chenye uwezo wa 35MVA.

"Awali wawekezaji walikuwa na kikwazo cha umeme kwa sababu hakukuwa na kituo cha kupozea umeme katika mkoa wetu na sasa changamoto imeisha hivyo kila mwananchi awaze kuwekeza katika maeneo tofauti ili kuweza kujijenga zaidi kiuchumi,".

PICHA: Muonekano wa eneo la mradi wa kupokea, kupoza na kusambaza umeme Inyonga chenye uwezo wa 15MVA na Mpanda chenye uwezo wa 35MVA unaotarajiwa kuanza kutumika Mei 20, mwaka huu.

Ameongeza kuwa ni wajibu wa wananchi kuilinda na kuitunza miundombinu uliyojengwa ili isichakae mapema pamoja na kuwahakikishia wananchi kuwa serikali kupitia wakala wa umeme vijijini Rea imeendelea kufikisha huduma ya umeme katika maeneo na vijiji na sasa hudumia hiyo imefika katika vitongoji hivyo ni wajibu wa wananchi kutumua fursa hiyo kujiimarisha kiuchumi kupitia umeme katika vitongoji vyao.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi huo kwa niaba ya meneja wa Tanescomkoa wa Katavi Mhandisi Dalali Lunyamila amesema mradi unatekelezwa na serikali kwa fedha za ndani  ambapo gharama yake ni bilioni 164.15 ulioanza Septemba 2022 na unatarajiwa kukamilika Juni 2025 huku utekelezaji ukiwa umefikia 96%.

"Mradi huu mara baada ya kukamilika utawezeshaKuunganisha Mkoa wa Katavi na umeme wa grid ya Taifa.itawezesha wawekezaji wa ndani na nje kuwa na uhakika wa kupata umeme kwa maendeleo ya Viwanda, kilimo na matumizi ya kijamii pia mapato kwa shirika la umeme Tanzania yataongezeka kwa kuunganisha wateja wengi zaidi na hivyo kujikwamua kiuchumi". Amesema Lunyamila.



Mwisho.


Announcements

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • View All

Latest News

  • KATAVI KUANZA KUTUMIA UMEME WA GRID YA TAIFA MEI 20,2025.

    May 15, 2025
  • KATAVI YAZIDI KUNG'ARA UUZAJI WA KABONI

    May 13, 2025
  • MABADILIKO YA MAJIMBO YA UCHAGUZI

    May 12, 2025
  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
More Videos

Quick Links

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Related Links

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Location Map

Contact Us

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Postal Address: Box 235, Mpanda -Katavi

    Telephone: 025-2957108

    Mobile:

    Email: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Katavi RS . All rights reserved.