• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Katavi Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
  • Services
  • Administration
    • Departments
      • Adm and HR
      • Planning and Coordination
      • LGA.s
      • Infrustructures
      • EPSS
      • Water
      • Healthy
      • Education
    • Units
      • Information and Communication Technology
      • Finance and Accounts
      • Procurement and Management
      • Legal
      • Internal Auditor
    • Organization Structure
  • Publications
    • Guidelines
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events
  • Projects
    • Completed projects
    • On Going Projects
  • Districts
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Tourism
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

Kampeni ya Chanjo ya Matone ya POLIO yazinduliwa Mpanda, Mganga Mkuu wa Mkoa awataka Wananchi kutoa ushirikiano kwa timu za Wataalamu.

Posted on: May 19th, 2022

Pichani:Mganga Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt.Omari Sukari akishiriki kutoa Matone ya Chanjo ya POLIO kwa watoto chini ya miaka 5 katika Kituo cha Afya Ilembo Manispaa ya Mpanda alipozindua Kampeni hiyo ya Kitaifa Kimkoa 18 Mei 2022.

Na: John Mganga-IO Katavi RS

Kampeni ya Utoaji wa Chanjo ya Matone ya POLIO Kwa watoto wenye umri chini ya miaka 5 imezinduliwa rasmi Mkoani Katavi ikiwa ni utekelezaji wa Ratiba ya Kampeni ya Zoezi hilo Kitaifa

Katika Mkoa wa Katavi Kampeni hiyo inatekelezwa katika Wilaya za Mpanda,Mlele,Mpimbwe na Tanganyika ambapo uratibu wa Utoaji wa Matone ya Chanjo ya POLIO umeanza kutekelezwa katika ngazi za Halmashauri zote ndani ya ilaya hizo.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Katavi amezindua Kampeni hiyo kwa kushiriki kutoa chanjo ya Matone ya POLIO ambapo pia amepita baadhi ya nyumba na kutoa chanjo kwa watoto chini ya miaka 5 walioko majumbani katika baadhi ya Nyumba katika Kata ya Ilembo.

Akizungumza wakati wa Uzinduzi wa Kampeni hiyo katika Kituo cha Afya Ilembo kilichopo Manispaa ya Mpanda, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt.Omari Sukari ametoa rai kwa Wazazi,Walezi na Wananchi kwa Ujumla kutoa Ushirikiano kwa Timu za Wataalamu zinazopita nyumba kwa nyumba kutoa huduma hiyo ya Matone ya  Chanjo ya POLIO.

Amesema lengo la Mkoa ni kuhakikisha kuwa watoto wote wenye Umri chini ya Miaka 5 wanafikiwa na huduma hiyo na kwamba wamejipanga kuhakikisha kuwa maeneo yote yenye watoto kama vile Mashuleni,pamoja na vituo vya Malezi yanafikiwa.

Mganga Mkuu wa Mkoa ametoa wito  kwa Wananchi kupuuza Taarifa zote za Upotoshwaji zinazotolewa na watu wasio na nia njema na badala yake waelekeze maswali ya Ufahamu kwa wataalamu wa Afya wanaopita katika maeneo mbalimbali ili kutoa huduma ya Chanjo hiyo.

Kwa Upande wao Wazazi na walezi waliojitokeza katika kituo cha Afya Ilembo waliowaleta watoto wao wameishikuru Serikali kwa namna ambavyo imechukua hatua za Haraka za kuwakinga watoto na hatari ya Ugonjwa wa POLIO.

Mnamo 13 Mei 2022,Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko katika mkutano na Vyombo vya Habari alisema ni muhimu kwa Wananchi kwa Wananchi kutoa Ushirikiano katika kufanikisha utekelzaji wa Kampeni ya utoaji wa Chanjo ya Matone ya POLIO kwa watoto wote wenye umri chini ya miaka 5 ili kufikia azma ya Mkoa ya kuwachanja watoto 189,465.

Kampeni ya Utoaji  wa Chanjo ya Matone ya POLIO kwa watoto wenye Umri chini ya miaka 05 itadumu kwa muda wa siku nne baada ya kuanza 18 Mei 2022 ambapo inatarajia kumalizika ifikapo 21 Mei 2022.

 

Announcements

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • View All

Latest News

  • RC MRINDOKO ATOA WITO KWA VIONGOZI KUHAMASISHA MATUMIZI YA CHAKULA CHENYE VIRUTUBISHI ILI KUTOKOMEZA UDUMAVU.

    June 10, 2025
  • RC MRINDOKO AZINDUA MSIMU WA UNUNUZI WA PAMBA NA MAZAO MENGINE KWA MWAKA 2025/26

    June 09, 2025
  • RC MRINDOKO AKUTANA NA WAENDESHA BODABODA KATAVI, ATOA WITO WA AMANI NA USHIRIKI UCHAGUZI MKUU 2025.

    June 05, 2025
  • JAJI MKUU WA TANZANIA ASISITIZA UADILIFU NA USHIRIKIANO WA WADAU KATIKA UTOAJI HAKI.

    May 28, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
More Videos

Quick Links

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Related Links

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Location Map

Contact Us

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Postal Address: Box 235, Mpanda -Katavi

    Telephone: 025-2957108

    Mobile:

    Email: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Katavi RS . All rights reserved.