• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

Ujenzi wa Hospitali ya Mkoa

Start Date: 2018-05-31
End Date: 2022-11-14

Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa inaendelea kutekeleza mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi, kama ilivyoelekezwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa (MB) wakati alipokuwa katika ziara ya kikazi Mkoani Katavi tarehe 25 hadi 27 Agosti 2021. Utaratibu wa namna pande zote mbili zinavyoshiriki katika ujenzi wa Hospitali hiyo umeanishwa vyema katika Hati ya Makubaliano (MoU) ambayo imesainiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi.

Katika Hati ya Makubaliano (MoU) iliyosainiwa jukumu kubwa la Katibu Mkuu-Afya ni kuandaa bajeti na kufuatilia upatikanaji wa fedha kwa ajili ya kuendeleza ujenzi pamoja na kuingia mikataba yote ya ujenzi. Kwa upande wa Katibu Tawala Mkoa jukumu kubwa ni kusimamia matumizi ya fedha za ujenzi kwa kuratibu na kusimamia manunuzi ya vifaa vya ujenzi, malipo ya Mkandrasi na Malipo ya Mshauri Elekezi kupitia kamati alizoziunda kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huu pamoja na kusimamia na kufuatilia shughuli za ujenzi zinazoendelea kila siku.

Ujenzi wa Hospitali mpya ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi unatekelezwa kwa awamu kama ifuatavyo kulingana na upatikanaji wa fedha, awamu ya kwanza ya ujenzi wa mradi huu ilianza na majengo matatu ambayo ni Jengo kuu lenye ghorofa moja lenye Kitalu A na B litakalotoa huduma za afya ya uzazi mama na mtoto (Maternity), huduma za dharura (EMD), wagonjwa wa Nje (OPD), Famasi, huduma za Radiolojia, Huduma za upasuaji na huduma za uangalizi Maalumu (ICU) pamoja na jengo la Maabara. 

Utekelezaji wa ujenzi huu ulianza mwezi Mei, 2018 chini ya usimamizi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi ambapo ulikuwa utekelezwe kwa kipindi cha wiki 48 kwa gharama ya Tsh.9.7b. Aidha ilipofika Februari 2019, mradi ulikabidhiwa Wizara ya Afya ukiwa kwenye hatua ya msingi sawa na asilimia 20 ukiendelea kutekelezwa na Mkandarasi SUMA JKT kwa mfumo wa Kandarasi (conventional method). Mradi huu uliendelea kutekelezwa kwa utaratibu wa kandarasi mpaka mwezi April 2021 ukiwa katika asilimia 43 ya utekelezaji ambapo Tsh.3.6b zilitumika.  Serikali iliamua kubadilisha mfumo wa utekelezaji wa mradi huu kwenda kwenye mfumo wa “Force account” ili kuharakisha utekelezaji wa mradi huu.

ili kufanikisha utekelezaji wa mradi huu kwa utaratibu wa “Force Account”, Serikali kupitia Wizara ya Afya ilikamilisha taratibu za manunuzi za kumpata Mshauri elekezi na Fundi mjenzi ambapo Mshauri Elekezi ni Crystal consultant na Fundi mjenzi ni SUMA JKT, kwa sasa gharama za kukamilisha mradi huu zinakadiriwa kuwa Tsh.12b ambapo 1.98b ni gharama za ufundi atakazolipwa SUMA JKT na kiasi cha Tsh.10.2b kitatumika kumlipa Mshauri Elekezi na kununua vifaa vya ujenzi.

Mkandarasi alikabidhiwa site tarehe 15 Septemba 2021 kwa ajili ya kuanza shughuli za ujenzi na mradi ulipaswa kukamilika tarehe 14/11/2022, hata hivyo ujenzi haukuanza katika muda huo kutokana na changamoto za ucheleweshaji wa kibali cha matumizi ya fedha za ujenzi na taratibu za manunuzi ambapo zilipotea siku 58.  Muda wa ujenzi uliopangwa ni miezi 10, aidha mpaka sasa Serikali imeshatoa kiasi Jumla ya Tsh bilioni 9.28 kwa ajili ya kundeleza ujenzi , kwa sasa ujenzi unaendelea na uko katika hatua ya umaliziaji (ufungaji wa CT scan, ufungaji wa LIFT na ufungaji wa mifumo ya gesi tiba) Pamoja na kazi za nje, kiujumla utekelezaji wa mradi umefikia 98% kwa upande wa Wing A.  Hata hivyo Hospitali tayari imeshaanza kufanya kazi, kazi zilizobakia zinaendelea kushughulikiwa wakati huduma zikiendelea kutolewa.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MABADILIKO YA MAJIMBO YA UCHAGUZI

    May 12, 2025
  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved