• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

Posted on: April 24th, 2025

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Deogratius Ndejembi, amekutana na wananchi wa eneo la Western, sehemu iliyopo ndani ya Kitongoji cha Luhafwe, iliyotengwa kwa ajili ya uwekezaji na yenye ukubwa wa hekta 46,000 (sawa na ekari 115,000), katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika, mkoani Katavi. Lengo la mkutano huo limekuwa kusikiliza kero za wananchi na kuweka mikakati ya kutatua mgogoro wa ardhi unaolikumba eneo hilo.

Katika mkutano huo wa hadhara, Waziri Ndejembi ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imejikita katika kuhakikisha haki inatendeka kwa kila mwananchi bila upendeleo. Amesisitiza kuwa maamuzi yote yanayochukuliwa katika eneo hilo yanazingatia maslahi mapana ya wananchi na kulinda amani ya jamii.

Waziri Ndejembi amewahimiza wananchi kuendelea na shughuli zao za kilimo katika maeneo waliyonayo kwa sasa, hadi suluhisho la kudumu kuhusu umiliki wa ardhi litakapopatikana. Aidha, amekemea ongezeko la kaya mpya katika eneo hilo, akibainisha kuwa hatua hiyo inaweza kuongeza ugumu wa kupata suluhisho la mgogoro uliopo. Ametoa maelekezo kuwa wakazi wapya wanaotaka kuingia katika eneo hilo wafahamishwe kuhusu hali halisi na waelekezwe kutafuta maeneo mengine ya makazi.

Katika kuhakikisha mgogoro huo unapatiwa ufumbuzi wa haraka, Waziri Ndejembi amemwagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Mhandisi Anthony Sanga, kuunda timu maalum ya usuluhishi itakayochunguza suala hilo na kuwasilisha ripoti ya mapendekezo ndani ya wiki tatu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko, amemwelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika kufuatilia uwepo wa vitongoji visivyotambulika katika eneo hilo, tofauti na Kitongoji cha Luhafwe ambacho ndicho kinachotambulika rasmi. Pia amesisitiza kuwa mihuri feki inayodaiwa kutumika itambuliwe na ikabidhiwe kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ndani ya siku tatu.




Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MABADILIKO YA MAJIMBO YA UCHAGUZI

    May 12, 2025
  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved