• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

Wanne wasimamishwa kupisha Uchunguzi, Matumizi ya Milioni 300 Ujenzi Hospitali Nsimbo,

Posted on: September 17th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mhe. Mwanamvua Mrindoko, ameagiza kusimamishwa kazi watumishi wanne wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, kupisha uchunguzi wa   utata wa matumizi ya Sh milioni 300 za ujenzi wa mradi wa Hospitali ya Wilaya ya Nsimbo.

Maagizo hayo ameyatoa 17 Septemba 2022 mara baada ya kufanya ziara ya kukagua ujenzi wa hospitali hiyo, ambapo baada ya kupokea Taarifa ya Matumizi ya fedha za Ujenzi wa Hospitali hiyo alibaini utata katika matumizi ya Shilingi Milioni 300.

Waliosimamishwa kazi ni  pamoja na Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, Mkuu wa Idara ya Afya, Ofisa Mipango pamoja na mkaguzi wa ndani kwa kumdanganya kuhusu matumizi ya fedha hizo.

Pia amemuelekeza mkaguzi wa ndani wa Mkoa, pamoja wataalam wengine waliopo chini ya Katibu Tawala wa Mkoa, ndani ya siku saba kukagua Sh milioni 300, namna zilivyotumika, huku akitoa siku nyingine 30 kukagua miradi yote inayotekelezwa katika Halmashauri hiyo, ikiwemo vituo vya afya, shule na vituo vya tozo.

“Hii inaanza kunipa wasiwasi kwamba inawezekana hata hiyo miradi mingine kuna mambo ambayo hayaendi vizuri,” amesema RC Mrindoko.

Ameiagiza TAKUKURU Mkoa wa Katavi kukagua kwa undani mradi mzima wa hospitali ya Wilaya Nsimbo, ili kubaini ubadhirifu uliofanyika kuanzia matumizi ya fedha, ubora wa mradi, ununuzi wa vifaa na thamani zake na endapo watabaini wabadhirifu hatua kali za kisheria zichukuliwe.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Jamila Yusuf alimwambia mkuu wa Mkoa kuwa, Kamati ya Usalama Wilaya, baada ya kufuatilia matumizi ya Sh milioni 300, waliambiwa kiasi cha sh mil 210 zimetumika katika matumizi mengine nje na eneo lililokusudiwa, hivyo wakamuagiza mkurugenzi kufuatilia fedha hizo zilitumika vipi, lakini hakupata majibu.

“Hii milango unayoiona yote ilikataliwa na aliyekuwa Waziri wa Tamisemi, Ummy Mwalimu, hata kuridhia shilingi milioni 300 itoke kwa ajili ya kufanya umaliziaji ni pamoja na kutengeneza milango, ambayo unaiona hadi leo bado ipo, mimi ninachojua hiyo fedha haikutumika,” alisema DC Jamila.

Hata hivyo imeonekana katika ukaguzi wa ujenzi wa mradi huo, kwa nyakati mbalimbali baina ya Kamati ya Usalama ya Wilaya, Mganga Mkuu wa Mkoa pamoja na Mkuu wa Mkoa wote walipokea taarifa zisizofanana.

“Sisi tulivyokuja na kamati yako iliyokuja kukuwakilisha, maelezo tuliyopewa na uliyopewa wewe leo ni tofauti kabisa, sasa sielewi aliyedanganywa kati yetu ni nani, lakini nadhani umedanganywa wewe mheshimiwa Mkuu wa Mkoa,”alisema DC Jamila

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved