• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

WANAWAKE MKOANI KATAVI WASHIRIKI UPANDAJI MITI KUELEKEA MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI.

Posted on: March 3rd, 2025


Katika kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yatakayofanyika kimkoa tarehe 5 Machi 2025, wanawake wa mkoa wa Katavi wameungana katika zoezi la upandaji miti katika Shule ya Sekondari Mtemi Beda, Manispaa ya Mpanda. Zoezi hilo limebeba dhamira pana, likilenga si tu utunzaji wa mazingira, bali pia kuchochea uhamasishaji wa lishe bora kwa familia kama njia mojawapo ya kutokomeza lishe duni mkoani Katavi.

Akizungumza wakati wa shughuli hiyo, Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Bi. Fidensiana Mwanakulya, ameeleza kuwa upandaji miti, hasa miti ya matunda na lishe, ni hatua muhimu katika kuhakikisha upatikanaji wa chakula chenye virutubisho vya kutosha kwa familia. Amesisitiza kuwa jamii inapaswa kutambua umuhimu wa mimea katika kuboresha afya, hususan kwa watoto na wanawake wajawazito, ambao mara nyingi hukumbwa na changamoto za lishe duni.

Pamoja na kuhimiza suala la lishe bora, Bi. Fidensiana amewataka wanawake kuwa karibu na watoto wao kwa kuhakikisha wanazungumza nao mara kwa mara kuhusu changamoto wanazokutana nazo katika maisha yao ya kila siku. Ameeleza kuwa malezi bora na mawasiliano ndani ya familia ni msingi wa kizazi chenye afya bora na maadili mema.

"Wanawake wana nafasi kubwa ya kulea kizazi chenye afya njema na kinachojitambua. Tusitumie muda wetu mwingi kwenye shughuli za nje na kusahau kuwapa watoto wetu malezi mazuri. Tuwaelekeze kuhusu lishe bora, afya, na maadili ili kuwajenga kuwa watu wenye manufaa kwa jamii," amesema Bi. Fidensiana.

Katika kuhitimisha hotuba yake, Bi. Fidensiana amewataka wanawake wa Katavi kushiriki kikamilifu katika shughuli zote za kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, huku akisisitiza umuhimu wa mshikamano katika kujenga jamii yenye afya na maendeleo.

Maadhimisho haya yanatarajiwa kuleta mijadala na shughuli mbalimbali zitakazolenga kuinua nafasi ya wanawake katika maendeleo ya jamii, huku suala la lishe bora likipewa msisitizo maalum kama njia ya kuhakikisha familia zenye afya na ustawi.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • RATIBA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI - MWAKA 2025 April 28, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA SEKTA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI MKOA WA KATAVI August 27, 2025
  • TAARIFA YA MAENDELEO YA SEKTA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI MKOA WA KATAVI August 27, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AKAGUA MIRADI YA MAJI MPANDA, ATOA MAAGIZO YA KUONGEZA KASI YA UTEKELEZAJI.

    September 03, 2025
  • RC MRINDOKO AHIMIZA AMANI NA USHIRIKIANO KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025.

    September 01, 2025
  • MFUMO WA E - MABORESHO KUIMARISHA UTENDAJI KWA WATUMISHI WA UMMA.

    August 26, 2025
  • MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA YAFIKIA TAMATI, DC BUSWELU AWASISITIZA UZALENDO

    August 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved