• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

SAMIA DAY; KUADHIMISHA MIAKA MITANO YA MAFANIKIO YA SERIKALI YA AWAMU YA SITA KATAVI

Posted on: July 2nd, 2025

Mkoa wa Katavi umeanda tamasha kubwa la Samia Day ili kutangaza Mafanikio ya Serikali yaliyopatikana kwa kipindi cha miaka 5 ya Uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Tamasha hilo linatarajiwa kufanyika kuanzia Juni 4, hadi 05, 2025 katika Viwanja vya Shule ya Msingi Inyonga vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlele ambapo mgeni Rasmi atakuwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mheshimiwa Mwanamvua Hoza Mrindoko.

 

PICHA: Katibu tawala Mkoa wa Katavi Albert Msovela akizingumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kutambulisha Tamasha la Samia Day.

Akizungumza na waandishi wa habari Katibu tawala mkoa wa Katavi Albert Msovela leo Juni amesema kuwa lengo ni Kumpongeza na kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa mchango wake wa kuleta fedha Zaidi ya Trilioni 1.3 ambazo zimesaidia kutekelezwa kwa miradi mingi ya maendeleo Mkoani Katavi katika Sekta zote za maendeleo na huduma kwa Jamii.

“Kauli mbiu katika inayobeba tamasha hilo “Asante Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa fedha za Maendeleo, Katavi Imara na Maendeleo Imara” likihusisha Serikali ya Mkoa wa Katavi, Taasisi zote na kwa kushirikiana na timu kizimkazi maarufu kama Mkasi Utaongea,”. Amesema Msovela.  

Amesema kuwa Juni 04,2025 TIMU KIZIMKAZI (Mkasi Utaongea), Viongozi na Wataalam watapata fursa ya kutembelea Hifadhi ya Katavi pamoja na kujionea uzuri wa asili wa mbuga ya Katavi national park, Kuona miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo Mradi wa Maji wa Miji 28 uliopo Shanwe, Vihenge vya kuhifadhia mazao, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa na kituo cha kupozea umeme wa Grid ya Taifa.

Aidha Kutakuwa na Usiku wa Mama Samia tukio litakalofanyika katika ukumbi wa Mpanda Social Hall ambapo baadhi ya Viongozi watapata fursa ya kuongea na kubadilishana mawazo kuhusu Mkoa tulipotoka, tulipo kwa sasa na tunakoelekea.

PICHA: Katibu tawala Mkoa wa Katavi Albert Msovela akizingumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kutambulisha Tamasha la Samia Day.

Msovera ameongeza kuwa Tarehe Juni 5, 2025 itakuwa kilele cha Samia Day ambapo yataanza Matembezi ya hiari kuanzia Saa 01:30 asubuhi ambayo yatafanyika katika Mji wa Inyonga Wilayani Mlele ambayo yataongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mheshimiwa Mwanamvua Hoza Mrindoko.

“Michezo itakayofanyika itajumuisha Mpira wa Miguu, Kuvuta Kamba, Kukimbia na Magunia, Kufukuza kuku na Mbio za mita 100 hivvyo tunawaomba Wananachi kujitokeza kwa wingi kushiriki katika tukio hilo muhimu na la kihistoria katika Mkoa wetu.

PICHA: Katibu tawala Mkoa wa Katavi Albert Msovela akizingumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kutambulisha Tamasha la Samia Day.

Ameongeza kwa makundi yote katika Jamii wakiwemo Bodaboda, Wasanii, Bajaji, Mama Lishe, Machinga na makundi mengine kujitokeza kwa wingi katika Matembezi ya Hiari na maadhimisho yote kwa ujumla. Vilevile, Taasisi zote za Serikali na zisizo za Serikali, Mashirika ya Kiraia, Sekta binafsi na Wadau wa maendeleo kujumuika pamoja katika siku hiyo.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • SAMIA DAY; KUADHIMISHA MIAKA MITANO YA MAFANIKIO YA SERIKALI YA AWAMU YA SITA KATAVI

    July 02, 2025
  • WANUFAIKA TASAF WAJIVUNIA MAFANIKIO.

    June 27, 2025
  • RAS MSOVELA AAGIZA MAAFISA BIASHARA KUSIMAMIA ELIMU KWA WAFANYABIASHARA, MIKATABA YA WAWEKEZAJI NA ULINZI WA MAENEO YA UWEKEZAJI.

    June 26, 2025
  • RC MRINDOKO ASISITIZA UWAJIBIKAJI KATIKA KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

    June 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved