• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

RC MRINDOKO AKUTANA NA VIONGOZI WA TABEDO KUJADILI MAENDELEO YA UFUGAJI NYUKI KATAVI

Posted on: January 2nd, 2025





Kikao Kati ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi na Viongozi wa TABEDO Kujadili Maendeleo ya Ufugaji Nyuki Tanzania.

Leo, Januari 2, 2025, kikao muhimu kimefanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi kati ya Mkuu wa Mkoa, Mhe. Mwanamvua Mrindoko, na viongozi wapya wa Chama cha Kuendeleza Ufugaji Nyuki Tanzania (TABEDO). Kikao hicho kimekuwa na dhima ya kuwatambulisha viongozi wapya wa TABEDO pamoja na kuwasilisha malengo na mikakati yao ya kuimarisha sekta ya ufugaji wa nyuki nchini.

Viongozi wa TABEDO wamemuomba Mkuu wa Mkoa kushirikiana na Halmashauri zote za Mkoa wa Katavi kuhakikisha wanachama wa chama hicho wanapata msaada wa pamoja na kuhakikisha vikundi vyote vya wafugaji wa nyuki ndani ya mkoa vinajumuishwa rasmi kama wanachama wa TABEDO.

Rc Mrindoko, akizungumza katika kikao hicho, amesema kuwa Mkoa wa Katavi bado una fursa kubwa ya kuendeleza ufugaji wa nyuki kama shughuli ya kibiashara yenye manufaa kwa wananchi. Amebainisha kuwa mkoa umejipanga kuhakikisha sekta hiyo inapata kipaumbele cha juu, na ameongeza kuwa yapo maeneo mengi yanayoweza kutumika kuimarisha ufugaji wa nyuki kwa tija kubwa.

Aidha, ameongeza kuwa viongozi wa TABEDO wanapaswa kujipambanua kwa wadau wao wa chini, hususan wafugaji wa nyuki, na kuhakikisha wanajenga mnyororo wa thamani wa mazao ya nyuki kama asali na nta. Mheshimiwa Mrindoko kupitia kikao hicho kutoa wito kwa wawekezaji na wadau mbalimbali wenye nia njema ya kuwekeza katika sekta hiyo, akisisitiza kuwa Mkoa wa Katavi una uwezo mkubwa wa kuendeleza ufugaji wa nyuki na shughuli za uchakataji wa mazao hayo.

Ametoa hakikisho kwamba serikali ya mkoa itashirikiana kwa karibu na TABEDO na wadau wengine kuhakikisha sekta ya ufugaji nyuki inakua na kuchangia maendeleo ya kiuchumi kwa mkoa na taifa kwa ujumla.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved