• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

RC Katavi azindua ugawaji miongozo ya uboreshaji Elimu Awataka wadau kumaliza changamoto Sekta ya Elimu Katavi.

Posted on: September 12th, 2022


Viongozi wa Serikali pamoja na Wadau mbalimbali wa Elimu Mkoani Katavi  wametakiwa kujipanga ili kuhakikisha kuwa  wanaondoa kabisa changamoto mbalimbali zinazoikabili Sekta ya Elimu Mkoani Katavi.

Rai hiyo imetolewa Septemba 9, 2022  na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe Mwanamvua Hoza Mrindoko katika hafla ya uzinduzi  wa ugawaji wa miongozo ya uboreshaji wa sekta ya Elimu iliyofanyika katika Ukumbi wa Idara ya maji Manispaa ya Mpanda ikiwakutanisha wadau mbalimbali wa Elimu wakiwemo Viongozi mbalimbali wa Wilaya ya na Halmashauri.

Mhe.Mrindoko  ameeleza kikaoni hapo kuwa Licha ya Mafanikio makubwa ya Mkoa wa Katavi katika Sekta ya Elimu yaliyochangiwa zaidi na hatua mbalimbali ambazo Serikali ya awamu ya sita imezichukua katika  kuboresha Sekta ya Elimu Mkoani Katavi  ikiwemo uboreshaji wa miundombinu ya Elimu Kama vile Ujenzi wa madarasa na mengine mengi, bado jitihada za dhati  za wadau mbalimbali wa Elimu zinahitajika katika kuhakikisha kuwa changamoto mbalimbali zinazoendelea kuikabili  sekta ya Elimu Katavi  zinapatiwa ufumbuzi na kumalizwa kabisa.

“Sisi kama Mkoa bado tunayo changamoto ya Wanafunzi kukatiza masomo kutokana na sababu mbalimbali na wengine kushindwa kuendelea na masomo kutokana na Jamii inayowazunguka.Tunaendelea kupata watoto wanaochaguliwa kujiunga na Kidato cha kwanza na wanashindwa kuendelea.Katika hili kila mdau ana wajibu wa kuhakikisha kuwa hatuna mdondoko wa wanafunzi na kwamba ni wajibu wetu kama wadau kuhaikisha kuwa watoto wote wanaojiunga na kidato cha kwanza wanamaliza kidato cha nne”Alisema Mhe.Mrindoko.

 Mhe.Mrindoko pia amebainisha kuwa  ipo changamoto ya baadhi ya wazazi kuwazuia watoto kuendelea na masomo kutokana kisingizio cha kukosa uwezo na hivyo kuwataka Vingozi Ngazi zote kuhakikisha kuwa inafuatilia changamoto hiyo nbva kuchukua hatua stahiki kwa wale wote wanaozuia watoto kwenda Shuleni kwa kisingizio cha kukosa fedha ikiwa ni pamoja na kutoa Elimu kwa Jamii juu ya madhara ya kutowapeleka watoto Shuleni.

Mhe.Mrindoko amewaelekeza wakuu wa Wilaya Mkoani Katavi kuhakikisha kuwa wanatatua changamoto mbalimbali zinazoikabili Sekta ya Elimu ikiwemo kushughulikia changamoto ya wazazi wanaozuia watoto kuendelea na masomo kwa kuchukua hatua stahiki

Akifafanua zaidi kuhusu  miongozo hiyo Afisa Elimu Mkoa wa Katavi Dr.Elipidius Baganda amesema miongozo hiyo imeelezea namna mbalimbali ya kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoikabili Sekta ya Elimu ambapo kupitia miongozo hiyo itakayowafikia wadau wote wa Elimu katika ngazi ya Jamii itasaidia kwa sehemu kubwa kutoa muongozo wa namna ya kukabiliana na  kuondoa changamoto mbalimbali zinazoikabili Sekta ya Elimu ndani ya Mkoa wa Katavi lengo likiwa ni kuinua ubora wa Elimu Mkoa wa Katavi

Nao wadau mbalimbali walioshiriki katika uzinduzi huo wa Ugawaji wa Miongozo hiyo katika ngazi ya Mkoa wameeleza kuwa Wazazi na walezi ni wadau muhimu hivyo ni muhimu wazazi kushirikiana kwa karibu na Wazazi ili kuhakikisha kuwa watoto wanapata Elimu kama inavyotakiwa

“Kama wazazi watawawekea watoto misingi mizuri mpaka wanafika shuleni watakuwa na misingi mizuri lakini ushirikiano wa Walimu na wazazi ni kitu muhimu na endapo hakutakua na ushirikiano basi changamoto hizo zilizoainishwa katika miongozo zitaendelea hivyo ni jukumu letu kama wazazi na walimu kudumisha ushirkiano kwa ustawi mzuri wa watoto .” alisema Mwalimu Sabas Korongo.

Elizabeth Madenge Mwalimu kutoka Wilayani Mpimbwe amemshukuru Rais Samia kwa namna ambavyo anatoa kipaumbele katika Sekta ya Elimu  na kwamba amefarijika kupata miongozo ambayo inatoa dira ya namna ya kukabiliana na changamoto mbalimbali katika Sekta ya Elimu.







Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved