• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

RC Katavi apiga marufuku uoshaji wa Magari ndani ya Mito.

Posted on: October 10th, 2022

Pichani: Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko akimkabidhi zawadi ya Cheti Mkuu wa Wilaya ya Mlele Mhe.Filberto Sanga baada ya Wilaya ya Mlele kutangazwa kufanya vizuri katika suala la Utunzani wa Mazingira.


Mpanda- Katavi. 

Ili  kudhibiti uharibifu wa mazingira na kuzuia magonjwa ya mlipuko, Mkuu wa mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko amekemea vikali tabia ya baadhi ya  Wananchi kuosha vyombo vyao vya Moto ndani ya mito  na badala yake amewataka kutafuta maeneo mengine na kuweka miundombinu ya Maji ili kufanya kazi yao hiyo 

RC Mrindoko amepiga marufuku hiyo 10 Oktoba katika kikao cha tathimini ya utekelezaji wa mpango mkakati wa usafi na utunzaji mazingira mkoa wa Katavi,kilichowakutanisha Viongozi mbalimbali wakiwemo wa Dini, Serikali sambamba na wadau mbalimbali.

"Nimarufuku na suala hili lisimamiwe na likomeshwe kabisa. Tuache vyanzo vya maji vitumike kwa matumizi mazuri....hata kama utakuta gari langu pale limeandikwa RC Katavi,ukimkuta (Dereva) anaosha kule kamata hilo gari"

Katika kikao hicho kilichoongozwa na Mkuu wa Mkoa,wadau wamependekeza na kupitisha kila kaya kupatiwa miche 5 ya miti Kwa ajili ya  kupanda ili kuendelea kutunza mazingira sanajri na kila Taasisi kupewa miche kuanzia 20,hiyo ikiongezeka kutokana na ukubwa wa Taasisi husika kama TANROAD,TARURA,RUWASA n.k

Kupitia mkakati uliozinduliwa Mwezi April wa "Ngarisha Katavi,tunza mazingira" katika kipengele cha mazingira kikizitaka kila Halmashauri kupanda miche Milioni 1.5 kwa kila mwaka,RC Mrindoko ameziagiza Halmashauri zote kutekeleza agizo hilo kwa kuanzisha vitalu visivyopungua miche hiyo kwa kuwa ni takwa la kisheria na sera ya mazingira.

Katika hatua nyingine,RC Mrindoko amesainiana na kukabidhi mikataba ya Lishe na wakuu wa Wilaya za mkoa huo lengo likiwa ni utekelezaji wa kupambana na lishe duni kuanzia ngazi ya Wilaya hadi ngazi ya kitongoji.

Kutokana na tathimini ya Sita ya Mwaka 2021 ya Lishe, Mkoa wa Katavi uko nafasi ya 14 Kitaifa huku sababu ya nfasi hiyo ikitajwa kuwa ni pamoja na Halmashauri za Mkoa huo kushindwa kutoa fedha za afua za Lishe kama ilivyoainishwa kwenye Bajeti na mipango.

www.katavi.go.tz


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved