• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

RC Katavi aongoza Wananchi kupanda Miti,ahimiza utunzaji wa mazingira,vyanzo vya Maji,akemea vikali shughulli za kibinadamu katika vyanzo vya Maji.

Posted on: January 26th, 2023

Na:OMM Katavi.

Serikali Mkoani  Katavi imeendelea na utekelezaji wa  Agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dk Samia Suluhu Hassan la kupanda miti ambapo takribani  miti  Milioni 4.7 imepandwa katika meneo mbalimbali  kupitia  kampeni Maalumu  ya Ng'arisha Katavi tunza mazingira  iliyoanza Tarehe 24/1/2023.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko 26 Januari aliwaongoza Viongozi na Wananchi Mkoani humo kupanda Miti katika Bwawa la Mto Milala Manispaa ya Mpanda  ikiwa ni uzinduzi rasmi wa Kampeni endelevu ya Upandaji wa Miti almaarufu “Ng'arisha katavi tunza Mazingira” iliyoanza kutekelezwa katika ngazi ya Wilaya Tangu 24 Januari 2023.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa Kampeni hiyo ya Upandaji mti Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amesema Hadi sasa takribani miti 4.7 imepandwa katika maeneo mbalimbali Mkoani humo ambapo lengo ni kufikia lengo la Upandaji wa Miti Milioni 10 kwa Mwaka 2023.

“Kwa mwaka 2023 lengo letu ni kupanda miti Milioni 10 mpaka sasa tumepanda miti zaidi ya milioni 4.7 kwenye halmsahauri zote kwenye taasisi za shule msingi na sekondari pamoja na kaya za mtu mmoja mmoja'' amesema Mrindoko.

Mkuu wa Mkoa Mrindoko amewahimiza  Wananchi Mkoani Katavi kuendelea kupanda miti katika maeneo yao ya makazi ikiwa nisehemu ya kuunga mkono juhudi za serikali katika utunzaji wa Mazingira.

Mrindoko akiwa katika Bwawa la Milala amepiga marufuku kufanya Kazi yeyote ya kibinadamu kwenye chanzo hicho kwa kuwa ndicho chanzo kikuu Cha maji katika Mradi wa maji wa miji 28 ambao mkoa wa katavi nisehemu ya wanufaika na Mradi huo pindi utakapoanza kutekelezwa.

“Nitumie nafasi hii kupiga marufuku na kukataza kabisa shuguli za kibinadamu kuzunguka Bwawa la Milala kulima,Kuchunga Ngo”mbe,Kufuga,Kuvua Samaki,na kufanya shuguli nyingine ni marufuku nimesema bwawa hili ni bwawa mhimu nichanzo cha maji na ttutakilinda na kukitunza kwa kushirikiana na wanachi waliopo maeneo haya”

Katika hatua nyingine amewaomba wananchi walio karibu na Chanzo hicho  Bwawa  la Milala kuwa Mabalozi na walinzi wa vyanzo hivyo Kwa kutoa taarifa za Kwa mamlaka husika kama Kuna kiashria Cha uharibu wa mazingira na vyanzo vya maji kwenye bwawa Hilo zinazofanywa na binadamu.

Awali akitoa taarifa Kwa Mkuu wa mkoa wa Katavi Kaimu  Mkurugenzi wa Muwasa Manispaa ya Mpanda Justini Wambali amesema katika kulinda chanzo hicho Cha maji wamekuwa wakishirikiana Kwa pamoja  na wananchi kukilinda chanzo hicho kwa kutokufanya shughuli za kibinadamu.

Wambali ameeleza kuwa katika Mradi wa maji wa miji 28 utakwenda kuwa mkombozi wa utoaji wa huduma ya maji kwa wanachi wa Manispaa ya Mpanda kwani tayari mikataba baina ya serikali na wafadhili kutoka Serikali ya India  ulishasainiwa tayari kwa utekelezaji kwa Gharama ya shilingi Bilioni 22.

"Mradi wa ujenzi wa Bwawa la Milala unakwenda kutatua kero ya upatikanaji ya huduma ya maji kwa wananchi wa Manispaa ya Mpanda kwa asilimia mia moja kwa kuongeza uzalishaji wa maji kutoka Lita Milioni 6 na elfu 50 kwa siku hadi kufikia lita Milioni 19 na elfu 50 kwa siku ambapo mahitaji ya maji kwa kata 15 za Manispaa ya Mpanda ni lita Milioni 15".

Amesema Kwa Sasa bwawa Hilo linatumika kama chanzo cha Maji Kwa kutoa huduma ya maji katika baadhi ya maeneo ya kata ya shanwe na Eneo la chuo Cha Veta Mpanda.

Hamisi Mrisho mkazi wa Bwawani amesema aungamkono agizo la mkuu wa Mkoa la kupiga marufuku kazi za kibinadamu kwenye Bwawa la Milala  na kuhakikisha wao kama wakazi wa eneo jirani na chanzo hicho cha bwawa watakuwa sehemu ya kulinda na Kutunza vyanzo vya Maji kwa vitendo.

‘’Kwa kuwa zoezi hili la upandaji miti ni endelevu naunga mkono agizo la Mkuu wa mkoa” amesema Mrisho.

Kwa upande wake Anjelina Lucas mkazi wa kivukoni  akiwa katika chanzo hicho Cha maji Cha bwawa la Milala amesema Kila mwanananchi anawajibu wa kutunza Mazingira Ili kulinda vyanzo vya maji.

"Tumeshiriki kupanda miti kwenye Bwawa hili  na sisi kama wananchi tupo Pamoja na Serikali kutunza rasilimali maji Kwa kutunza Mazingira na kupanda miti’’ .

Kampeni ya kupanda miti katika mkoa wa katavi inayojulikana kama Ng'alisha katavi tunza Mazingira inalengo mahususi ya kulinda mazingira na vyanzo vya maji kama sehemu ya tekelezo agizo la Serikali la kupanda miti kama sehemu ya kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC MRINDOKO AZINDUA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU (GAWE) 2025

    May 05, 2025
  • RC MRINDOKO AIHAKIKISHIA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MKOANI KATAVI.

    April 29, 2025
  • WAZIRI NDEJEMBI AONGOZA MIKAKATI YA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI ENEO LA WESTERN, KITONGOJI CHA LUHAFWE – H/ WILAYA YA TANGANYIKA

    April 24, 2025
  • PPPC WATOA ELIMU UIBUAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA UBIA.

    April 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved