• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

MRINDOKO AHIMIZA UBUNIFU NA ABAINISHA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOANI KATAVI.

Posted on: August 6th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Hoza Mrindoko, amehimiza wafanyabiashara na wadau wa maendeleo kuongeza ubunifu katika bidhaa na huduma wanazozalisha, ili kuongeza ushindani wa kibiashara na kuchochea ukuaji wa uchumi mkoani Katavi.

RC Mrindoko ametoa msimamo huo wakati akitembelea mabanda ya washiriki kutoka Katavi katika maonesho ya kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya. Ametumia fursa hiyo kusisitiza kuwa ubunifu na matumizi ya teknolojia ni nyenzo muhimu kwa mkoa huo kufikia maendeleo ya haraka.

Katika ziara hiyo, RC Mrindoko ameambatana na viongozi mbalimbali wakiwemo Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika, Mheshimiwa Onesmo Buswelu, Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Mheshimiwa Jamila, na Mkuu wa Wilaya ya Mlele, Mheshimiwa Alhaji Majid, pamoja na wakurugenzi wa halmashauri, wakuu wa idara na wataalamu kutoka mkoani Katavi.

Aidha, Mkuu huyo wa mkoa ametangaza fursa za uwekezaji zinazopatikana mkoani Katavi, akieleza kuwa sekta za kilimo, ufugaji, biashara, usafirishaji na mawasiliano zinahitaji wawekezaji zaidi kutokana na mazingira mazuri ya miundombinu na utayari wa serikali kushirikiana na sekta binafsi.

Katika maelezo yake, amebainisha maeneo maalum ya uwekezaji ndani ya Wilaya ya Tanganyika, yakiwemo Bandari ya Karema inayofungua fursa za kibiashara kupitia Ziwa Tanganyika, biashara ya kaboni, shughuli za uvuvi, pamoja na kilimo na ufugaji ambapo zaidi ya hekta 46,000 zimetengwa rasmi kwa ajili ya wawekezaji.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika, Mheshimiwa Onesmo Buswelu, ameeleza kuwa wilaya yake imejipanga vizuri kuweka mazingira rafiki kwa wajasiriamali na wawekezaji wa ngazi zote. Ameongeza kuwa Wilaya ya Tanganyika imenufaika na zaidi ya shilingi bilioni 500 kutoka Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa ajili ya miradi ya maendeleo inayowanufaisha wananchi wa Katavi.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI DESEMBA 2024 December 12, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2025 December 16, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 January 04, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • BENKI YA CRDB YATOA MSAADA WA MADAWATI SHULE YA WASICHANA KATAVI

    August 12, 2025
  • RC MRINDOKO AZIAGIZA HALMASHAURI ZOTE KATAVI KUSAMBAZA MBEGU BORA ZA UFUTA KWA WAKULIMA ILI KUONGEZA UZALISHAJI MSIMU UJAO.

    August 08, 2025
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA MPANDA YANG’ARA NANENANE 2025, YASHIKA NAFASI YA TATU.

    August 08, 2025
  • MRINDOKO AHIMIZA UBUNIFU NA ABAINISHA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOANI KATAVI.

    August 06, 2025
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI
  • KATAVI RS HABARI
  • KATAVI RS HABARI YOUTUBE

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved